Mlinzi wa kulia wa klabu ya Arsenal Bacary Sagna ameshindwa kukataa kuwa yu karibu karibu kurudi nyumbani kwao ufaransa huku akipigiwa upatu wa kujiunga Paris Saint-Germain au Monaco wakati wa kiangazi .
Kandarasi ya mchezaji huyo wa kimataifa wa ufaransa inakwisha msimu ujao japokuwa anatarajia kuongeza kandarasi ya mwaka mmoja zaidi , Kijana huyo mwenye miaka 30-anaoneka kuwa wazi kuwa anaweza kuondoka klabu hapo.
"Yeah najiskia raha kuona PSG inanihitaji ni klabu inayovutia wengi ," Alinukuliwa katika Le 10 Sport.
"Binafsi sijawasiliana na PSG Na sijui kama wameongea na wakala wangu au ni tetesi tu .
"Pale Arsenal, Hasa kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kila mtu ananieleza kuwa nitaondoka na kwenda PSG,Lakini hizo ni fununu tu ,sijui nini kitakwenda kutokea .
"Nina weza kuongeza kandarasi yangu hapa London lakini naweza kuondoka pia mwishoni mwa msimu .bado nina mwaka mmoja umesalia Tusubiri tuone .
"Kwa sasa natazama nini kitafuata klabuni kwangu na . Nafikili nahitaji kuonana wakurugenzi juu ya kuongeza kandarasi yangu lakini Monaco inaweza kuwa changamoto mpya siko karibu na PSG ,lakini ni Monaco au Arsenal.
No comments:
Post a Comment