16 January 2013

Pep Guardiola:KUANZA KAZI MSIMU UJAO Bayern Munich

Pep Guardiola

Klabu ya Ujerumani ya  Bayern Munich imetangaza kuwa Mkufunzi wa zamani wa Barcelona  Pep Guardiola ataichukua timu hiyo mwishoni mwa msimu  

Kijana huyo mwenye  miaka 41 alikuwa akihusishwa na kujiunga na  Chelsea na Manchester City - amatia saini kandarasi ya miaka mitatu mpaka  2016.
Guardiola atakuwa anaziba nafasi ya   Jupp Heynckes,ambaye anastafu mwishoni mwa msimu 
 
Bayern kwa sasa wako juu kwa Alama tisa zaidi wakiongoza ligi na wanatarajia kukutana na Arsenal mwezi ujao katika hatua ya kumi na sita bora ya ligi ya mabingwa .

Heynckes, 67, aliimbia klabu hiyo kabla ya  Christmas kuwa Hato ongeza kandarasi baada ya majira ya kiangazi .
Mkurugenzi mkuu wa Bayern'  Uli Hoeness Amesema kuwa : "Tunahijati Mkufunzi wa aina ya  Guardiola' ndiye anayeweza kuichukua nafasi ya  Jupp Heynckes."

No comments:

Post a Comment