13 May 2013

Massimiliano Allegri LAZIMA TUONGEZE ADHABU YA UBAGUZI !!

AC Milan's Mario Balotelli reacts to racist abuse from the visiting Roma fans at the San Siro on Sunday.
Mchezaji wa timu ya soka ya AC Milan  Mario Balotelli amekumbana na kadhia ya ubaguzi wa rangi kutoka kwa mashabiki na kusababisha mwamuzi   Gianluca Rocchi kusimsmisha  mtanganae huo katika kipindi cha pili baada ya kusimama kwa dakika kadhaa  katika kipindi hicho ilibidi watangaze kiwanjani  kuipinga tabia hiyo mchezo huo ulikwisha kwa timu hizo kwenda suluhu ya kutokufungana .

Kocha wa AC Milan  Massimiliano Allegri alisema baada ya mechi hiyo kuwa maamuzi ya maafisa kuisimamisha mechi bado hayakutosheleza ilibidi kuchukuliwa hatua zaidi .
"katika maoni yangu ,kuna suluhisho moja tu la kufanya inapotokea swala la ubaguzi ni kuvunja mechi  ," Allegri amezungumza hayo katika tovuti ya klabu hiyo .
"kuonyesha msisitizo kwa tatizo hili ni kutoa mamuzi makubwa zaidi . tunaweza kuadhibu watu siku za usoni na itatusaidia  kama taifa siku zijazo na kuonyesha uungwana .

No comments:

Post a Comment