13 June 2013

FABREGAS AIKATA MAINI MANCHESTER UNITED

Ndoto za Klabu ya Manchester United  kutaka kumsainisha mchezaji wa kimataifa wa uispania na Barcelona zimezimwa baada ya Cesc Fabregas kusema kuhama klabu yake ya sasa litakuwa jambo la Ajabu
Tangu  Fabregas arejee  Barca kutoka  Arsenal mwaka  2011 ameshindwa kabisa kuwa katika kiwango chake cha siku zote hasa katika timu ya kwanza jambo lilofanya kuibua habari kuwa   Manchester United wapo katika mstari wa mbele kumnyakuwa mchezaji huyo na kujipa kipaumbele kumsainisha.

japokuwa kiungo huyo , amekuwa makini kutaka kuchukua namba katika kikosi cha kwanza na ameonekana akiongea na Gazeti la Marca leo .

"Nimeshasema kuwa nafurahi kuwa hapa.yoyote atakayesema naondoka hanijui vizuri na hajawahi kuongea na mimi ," anaongeza kijana huyo mwenye miaka  26-.
"Hakuna jambo kutoka kwa wakala wangu,kwa sababu anajua kuwa sipendi watu nwengine wazungumze kuhusu mimi .Nafanya mambo yangu kibinafsi  na siongei kuhusu mambo haya na familia yangu  .
"kama kuna mtu yeyote anasema lolote kuhusu kitu ambacho akipo kuwa nataka kuondoka barca litakuwa jambo la ajabu .

No comments:

Post a Comment