10 June 2013

JULIO SIPENDI KIEMBA AENDE YANGA (SIKIZA SAUTI YAKE )


 

 Kocha msaidizi wa klabu ya soka ya Simba Jamhuri Kiwelu Julio amesema hapendi Kiungo wa Timu hiyo  Amri Kiemba kuwa  hapendi kuona mchezaji huyo anakwenda kwa mahasimu wao Dar es salaam Yanga afrikans ambao ni mabingwa wa Tanzania .

Amesema dhahiri kuwa hapendi kuona mchezaji huyo Akihamia Yanga  lakini akasisitiza kuwa hawezi kumpangia kwakua Kiemba ni Mtu mzima na ana haki ya kufanya Maamuzi yake Binafsi, amesema mchezaji huyo aliyewahi kuchezea klabu hiyo yanga na kuhamia Simba inaonekana anarejea katika klabu yake ya zamani ya yanga kiemba kwa sasa yupo kambini na timu ya taifa ya Tanzania ambayo inashirki michuano ya kufuzu fainali za kombe la dunia ikitokea moroco baada ya kufungwa  Mabao mawili kwa moja kule Marakesh ambapo mchezaji huyo  ndiye aliyefunga goli la kusawazisha kwa shuti la Mbali.

 Julio amesema hayo alipokuwa akiongea na moja ya kituo cha radio hapa nchini kuhusu uamuzi wa mchezaji huyo na kile kinachosadikiwa kuwa amekwenda klabu ya Yanga  .


SIKIZA HAPA 

 

1 comment: