HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

12 July 2013

Quinton Fortune AKWEPA MAFUA SIMBA NA YANGA AIONA DUNIA YA SOKA AZAM FC

 

 Quinton Fortune, Mchezaji wa zamani wa Manchester United ambaye kwa sasa anasomea fani ya ualimu wa soka kwenye kompaundi ya Manchester United alipotembelea Azam FC Chamazi leo kwa mwaliko wa DHL

Fortune alishangazwa na ubora wa Center ya Azam FC na kusema hajawahi kuona kitu kama hiki kinachomilikiwa na klabu hata kwenye nchi yake ya Afrika ya Kusini Hakuna..

Kauli hii ya fortune hainishangazi labda jambo ambalo lingenishangza kama angeenda kuziona zile klabu zangu mbili zinazo pigizana kelele utafikili wapo kwenye uchuuzi wa samaki pale feri au kariakoo 

Klabu hii za Azam ambayo nakumbuka wakati ikitafuta kupanda daraja kuna wakati nilikuwa nakutana na gari yao maeneo ya kigogo lakini sasa napishana na mabasi makubwa .

Hili ni jambo la kujivunia kwa sababu Leo nilipata bahati kubwa ya kuzungumza na jaffar Iddy alikuwa akinieleza kile ambacho Fortune aliwaambia kuwa ata yeye mwenyewe wakati anaingia Man utd Hakuamini lakini aliawaeleza wchezaji wa Azam walipata nafasi ya kumuuliza maswali na mengi lakini cha msingi ni kuwa Azam fc walimfurahia zaidi , Jaffar Iddy  kwa kua anatoka Bara la Afrika na ametembelea klabu hiyo ambayo wakati anachezea Man u  
Azam Fc haikuwepo pengine ilikuewepo kwenye makalatasi lakini alipoondoka Man u Azam fc ilianza kuonyesha Dalili za kuonekana.

Yapo mambo mengi ambayo Fortune ameyaona Azam fc na kudiliki kusema kuwa hata Nchini kwake hakuna klabu inayofanya jambo kama hilo kiasi cha kuuliza kuwa hii timu ni ya mtu au ya wanakikijiji 
lakini ni ya mtu Binafsi jambo lililomfanya achanganyikiwe zaidi.
   
  
Hivi tugeuze kiswahili kwa mfanooo Teh teh teh angekwenda simba ingekuaje nafikili angekutana na haya :- jambo la Kwanza kuruka viunzi vya nyanya zinauzwa pembeni ya klabu hiyo kelele za honi za magari harufu mbaya za mitalo iliyokithiri kwa harufu mbaya ambazo hata mbuzi hawezi kustaamiri kunusa Bila kusahau matusi ya Nguoni kutoka kwa wachuuzi wadogo wadogo wa simu na kelele za majenetreta ya umeme yanayo pambana na mgao usio kwisha katika mmtaa wa Agrey .

Kwenye Jengo sasa Kidogo Mh Mbunge  angeweza kujitetea kuwa aliichukua klabu ikiwa katika  
Hari mbaya na sasa anafanya marekebisho kwani unapoaingia getini katika klabu ya simba jengo la mkono wa kulia ndio linalo oonekana lina uafadhari la mkono wa kushoto sasa sina hata haja ya kulizungumzia lakini sijapita siku nyingi kwa kuogopa mafua yasiyo tibika inawezekana wametengeneza japo nakuwa Toamaso katika swala hilo.

Sasa shughuri na majibu ya kigugumuzi ingekuwa hapa Fortune angeomba kwenda kuona Academy na uwanja wa kufanyia mazoezi ya simba  majibu yangekuwa hapa hivi 
Kimombo (Yah Fortune You know ,,yeah the the stadium is is very Problem from hear i mean far away) majibu mengi ya kujigonga gonga sema tu hatuna kiwanja baba .


  
Lakini Fortune Huyu huyu kama angeenda Yanga yaani maskani ya klabu ya yanga   kule mtaa wa twiga na jangwani angeweza kukutana na mipango isiyokwisha na iliyojaa siasa nyingi bila shaka angekutana GYM ambayo bado tunamashaka kama inafanya kazi mpaka sasa kiofisi sio haba lakini Academy hakuna pengine wangemuonyesha uwanja wao ambao wanashindwa hata kumwagilia maji ili  uote nyasi.

Bila shaka Fortune atakaporejea Manchester kuendelea na masomo ataikumbuka Azam fc na  kuifurahia na huenda siku zijazo ubingwa wa Tanzania unaweza kuelekea mbagala .
Jambo kuu na la kipekee Azam fc inaifanya timu hii ionekane kama iko ulaya wakati iko Tanzania tena mbagala maeneo ya Chamazi na  nina Diliki kusema na kukubali  msemo wa kitabu ninacho kiamini cha Biblia  kuwa wale walio kuwa wa kwanza watakuwa wa  mwisho na wale walio kuwa wa mwsiho watakuwa wa kwanza 
Hiki ndio kifo Cha Simba na Yanga Well Done Azam fc   

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers