17 September 2013

KAYUNI AZIDI KUUULA

 
 
Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
 Tanzania (TFF),
 Sunday Kayuni 
atashiriki warsha ya
 wakufunzi 
wa 
makocha wa Shirikisho 
la Mpira wa
 Miguu Afrika (CAF)
 itakayofanyika 
kuanzia Oktoba 22-24 
mwaka huu.
 
Warsha hiyo 
iliyoandaliwa na 
CAF kwa ajili ya wakufunzi wake 
itafanyika nchini Cameroon.
 Wakufunzi 18 wa CAF kwa upande wa makocha watahudhuria 
warsha hiyo.
 
Madhumuni ya warsha hiyo
 ni kuainisha majukumu yao,
 kubadilishana uzoefu. 
Pia kuwapa methodolojia mpya ya ufundishaji na 
muongozo kuhusu mfumo wa leseni za makocha
 ambao watautumia katika nchi wanazotoka.
 
Mbali ya Kayuni Tanzania,
 wakufunzi wengine ni Ahmed Babiker 
(Sudan), Amadou Shaibu (Nigeria), 
Boy Bizzah Mkhonta (Swaziland), 
Duodu Fred Osam (Ghana), Edussei 
Anthony (Ghana), Fathi Nossir 
(Misri), Faouzy Altaisha (Sudan) 
na Fran Hilton Smith (Afrika Kusini).
 
Wengine ni Francis Oti-Akenteng 
(Ghana), Honour Janza (Zambia),
 Kasimawo Laloko (Nigeria), 
Mahmoud Saad (Misri), Paul 
Hamilton (Nigeria), Serame 
Letsoaka (Afrika Kusini), 
Shawky Abdel Shafy (Misri), 
Thondoo Govinder (Mauritius) 
na Ulric Mathiot (Seychelles),
 

No comments:

Post a Comment