HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

28 October 2013

NAKUKABIDHI KATIBA ILINDE

Jamal Emil Malinzi ndiye Rais mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) baada ya kuibuka kidedea katika uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo kwa kupata kura 73 kati ya kura 126 zilizopigwa, dhidi ya mpinzania wake Athumani Nyamlani aliyepata kura 52 kwenye kinyang'anyiro hicho kilichohitimishwa usiku wa kuamkia leo katika jengo la NSSF la Waterfront jijini Dar es salaam.


Malinzi ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha soka cha mkoa wa Kagera ameshinda uchaguzi huo ikiwa ni mara yake ya pili kugombea baada ya kushindwa na Rais wa zamani wa TFF Leodgar Chillah tenga mwaka 2008.Nafasi ya Makamu wa Rais imenyakuliwa na Wallace Kiria aliyemshinda Ramadhani Nasib kwa kura 67 dhidi ya 52, wakati mgombea mwingine katika nafasi hiyo Imani Mahugila Madega kapata kuta 6.

Katika nafasi za Ujumbe; Kanda ya 13; kiungo wa zamani wa Simba SC Wilfred Kidau amepata kura 60 na kuwashinda Muhsin Said kura 50, Omar Abdulkadir kura 10 na Alex Kabuzelia kura nne.

Kanda 12; Khalid Mohamed Abdallah amepata kura 69 na kumshinda Davies Mosha aliyepata kura 54.


Kanda ya 11 Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amepata kura 78 na kuwashinda Riziki Majala kura tano, Twahir Njoki kura mbili, Juma Pinto kura 26 na Farid Mbaraka kura 14, Kanda ya 10 ameshinda Hussein Mwamba aliyepata kura 63, huku Charles Komba akipata nne na Stewart Nasima 58.


Kanda ya tisa Othman Kambi aliyepata kura 84 yeye amewashinda Francis Bulame kura 30, wakati James Mhagama aliyepata 93 amemshinda Zafarani Damoda aliyepata kura 11 na Kanda ya nane, Ngube Kiondo amepata kura 73 amemshinda Ayoub Nyaulingo kura 52.

Kanda ya Tano, Ahmed Iddi Mgoyi aliyepata kura 92 amemshinda Yussuf Kitumbo aliyepata kura 34, wakati Kanda Omar Walii Ali amepata kura 53 dhidi ya 19 za Ally Mtumwa.


Eley Mbise amepata kura 51 dhidi ya 53 kura 57 za Lamanda Swai.
Mbasha Matutu aliyepata kura 63, amembwaga Vesastis Ligano aliyepata kura 61, wakati Vedastus Lufano aliyepata kura 51, amewashinda Jumbe Odesa Magati kura 11, Mugisha Galibona kura 24 na Samuel Nyalla kura 39 na Kanda namba moja, Karilo Samson hakuwa na mpizani akapita moja kwa moja.


Rais mpya wa TFF Jamal Malinzi akiwa na Dream Team yake baada ya uchaguzi



Rais Mstaafu wa TFF LEodegar Chilla Tenga akimkabidhi mikoba Rais Mpya Jamali Malinzi akkisaidiwa na katibu mkuu Angetille Osiah.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini aliyemaliza muda wake,Leodger Tenga (kushoto) akimkabidhi Mpira Rais Mpya wa shirikisho hilo,Jamal Malinzi mara baada ya kutangazwa mshindi katika Uchaguzi uliofanyika jana na kumalizika usiku wa kuamkia leo,ambapo alimshinda mpinzani wake,Athuman Nyamlani kwa kura 73.uchaguzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Water Front jijini Dar es salaam.Katika uchaguzi huo nafasi ya Umakamu wa Rais ilichukuliwa na Walace Karia ambaye alifanikiwa kuwagaragaraza wapinzani wake Imani Madega na Ramadhan Nassib.


Rais Mpya wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini,Jamal Malinzi akizungumza machache na Wajumbe wa Uchaguzi huo mara baada ya kutangazwa Mshindi wa nafasi ya Urais wa TFF,usiku wa kuamkia leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Water Front,jijini Dar es Salaam.Kulia ni Makamu Mpya wa Rais wa TFF,Walace Karia.

Rais Mpya wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini,Jamal Malinzi akipongezana na Makamu Mpya wa Rais wa TFF,Walace Karia mara baada ya kuibuka Kidedea.



.Picha na FullShangwe Blog via MICHUZIBLOG

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers