25 May 2014

KOMBE LA DUNIA: GHANA YAWASIRI UHOLANZI KWA MAZOEZI

 



Kikosi cha Timu ya soka ya Taifa ya Ghana’s kimewasiri Rotterdam Jumapili ya kikitokea Accra,ambapo watafanya mazoezi ya siku tatu wakiwa nchini humo  .

Nahodha wa Timu hiyo  Asamoah Gyan, na wenzake  Andre Ayew, Jordan Ayew, Jonathan Mensah, Emmanuel Agyemang-Badu, Abdul Majeed Waris, David Accam, Samuel Inkoom, Albert Adomah and Jerry Akaminko wote wamo kikosini.

Wakati wachezaji wachache kama Mubarak Wakaso na  Stephen Adams Bado hawaja wasili kwasababu tofauti . Muntari naye hakuonekana  katika uwanja wa Ndege pindi  Black Stars walipokuwa wakikwea pipa la KLM wakielekea  Amsterdam wakitokea uwanja wa kimataifa wa Ndege wa  Kotoko .
Ghana itacheza na Netherlands siku ya Ijumaa 31 May huko  Rotterdam.

No comments:

Post a Comment