29 June 2014

JAMES RODRIGUEZI 28,50 AIMALIZA URUGUAY SASA USO KWA USO NA BRAZIL

Colombia's James Rodriguez scores a stunning volley


Colombia itapambana na  Brazil katika Robo fainali ya michuano ya Kombe la Dunia  2014 Baada ya Kuibamiza Mabao mawili  kwa sifuri yalyofungwa na  James Rodriguez na kuipatia Ushindi Dhidi  Uruguay.
Rodriguez, 22, alifunga la kwanza kwa ufundi wa aina yake baada ya kugeuka na mpira hewani kutoka Takriba Mita 20 au Yard 25 ambapo mpira huo uligonga chini ya Besera  na kutinga wavuni. 
Uruguay fans
Uruguay, ikicheza bila  Luis Suarez aliyefungiwa miezi minne,walikuwa wadhaifu  na muda mwingi wa Mchezo walikuwa wakilinda zaidi Goli  hasa katika Nusu ya Kwanza ya Mchezo .
Rodriguez alifunga tena kwa shuti kali na kufunga goli lake la Tano katika mashindano ya Kombe la Dunia. 
James Rodriguez
Uruguay walimailiza kipindi cha pili kwa nguvu kubwa lakini walishindwa kupunguza angalau Goli moja, Maxi Pereira's alijaribu kufanya kama alivyofanya Rodriguez lakini mpira uliishia mikononi mwa mlinda Mlango David Ospina ambaye baadaye alidaka mpira uliopigwa na   Edinson Cavani.

No comments:

Post a Comment