13 June 2014

NEYMAR AIPAISHA BRASIL AIKUTA RECORD YA JAIRZINHO NA RONALDINHO.



Neymar Alifunga magoli mawili ,huku moja likiwa ni la Penarty ya utata  , Wakati Brazil ikiitandika Croatia katika mechi ufunguzi ya Kombe la Dunia ambapo Brazil wao ni wenyeji wa michuano hiyo.

Mabingwa hao mara tano walikuwa nyuma katika Dakika za mwanzo Pale  Marcelo's alipojifunga goli katika harakati za kuokoa , baada ya mpira uliopigwa kwa kuparazwa na  Nikica Jelavic's na kuipa Croatia Goli la uongozi. 

Lakini Brazil ilisawazisha kwa shuti kali la  Neymar la mita  25 baada ya  kupokea mpira kutoka kwa  Oscar's aliyekimbia kwa kasi.
Neymar alifunga  kwa Pernaty mara baada ya   Dejan Lovren kufamfanyia faulo Fred,na baadae  Oscar kufunga goli tatu katika dakika za nyongeza. 

Croatia italia na  maamuzi ya mwamuzi kutoka japan ambaye maamuzi yake yanaweza kuwa ya kawa hoja kubwa Croatia kwa mwamuzi Yuichi Nishimura baada ya  Fred kujiangusha akiwa mbele ya  Lovren na mwamuuzi kumamuru kupigwa pernaty.

Neymar

No comments:

Post a Comment