HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

1 September 2012

YANGA YAIKANDAMIZA COAST UNION


  Mbuyu Twite, akijiandaa kumimina krosi mbele ya Nsa Job.
Katika mchezo huo Yanga imeshinda 2-1, ambapo Coast Union ndiyo walikuwa wa kwanza kuandika bao katika kipindi cha kwanza, ambalo lilidumu hadi kumalizika kwa kipindi cha kwanza na kufanya timu hizo kwenda mapumzi huku Coast ikiwa mbele kwa bao 1-0.
 Kipindi cha pili Yanga ilianza kucheza kwa presha na kasi iliyowachanganya zaidi Coast na kukosa mabao ya wazo na mipira mingine kigonga miamba. 
Alikuwa ni Ally Shamte aliyepiga krosi matata iliyounganishwa moja kwa moja na beki wa Cost, Phillip Kaila, aliyeruka na kuuweka kimiani katika lango lake. bao la pili liliwekwa kimiani na Said Bahanuzi, bao lililodumu hadi kumalizika kwa kipute hicho.


No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers