HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

28 November 2012

SERENGETI BOYS KUKWEA PIPA LEO ,KUAGWA JIONI HII






Timu  ya soka ya Taifa ya vijana waliochini ya miaka 17 'Serengeti boys' inatarajia kuondoka usiku wa leo kwenda nchini  Congo Braza ville kwa ajili ya mchezo wa marudiano.

 Timu hii inaondoka na msafara wa watu 27 ikiwa ni wachezaji 18 na viongozi tisa huku wakiwa na matumaini makubwa ya kusonga mbele baada ya mchezo wa awali uliochezwa nchini kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

 Serengeti boys ambayo imeundwa na wachezaji chipukizi waliopatikana kutokana na mashindano ya Copa Cocacola inabidi washinde  mchezo huo au sare ya mabao yoyote au isyokuwa na mabao  ili waweze kuandika historia ambayo haijawahi kuandikwa hapa nchini.

 Itakumbukwa kuwa Tanzania iliwahi kufuzu  fainali za mwaka 2005 lakini ikaondolewa na ikafungiwa baada ya kugudulika umri wa mchezaji Nurdin Bakari kuwa haukuwa sahihi  kimashindano .

  Kocha Mkuu wa timu hii Jakob Michelsen amesema timu yake ipo tayari kupambana na Congo Brazaville na anajivunia faida ya bao moja walilolipata nyumbani.

"Wachezaji wapo kamili na wana ari ya kushinda mchezo huo na kwa sababu nyumbani tulishinda tunaamini tutashinda pia", alisema Jacob

 Tunawatakia kila la heri mfanikiwe kufuzu fainali za vijana zinazotarajiwa kuchezwa nchini Morocco, Machi mwakani.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers