HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

27 February 2013

OUHOOO TFF HII SASA ISHAKUWA TABU FIFA SERIKALI YATIA MCHANGA SOKA TZ


http://mw2.google.com/mw-panoramio/photos/small/48666346.jpg

Baada ya serikali kutangaza juzi kuwa imeifuta katiba mpya ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kutaka itumike kwa katiba ya zamani iliyopitishwa mwaka 2006, Tanzania imejiweka katika hatari zaidi ya kufungiwa kuliko ilivyowahi kutokea wakati wowote kwani uamuzi huo unaweza kupingana moja kwa moja na kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), .
  Mmoja wa wanasheria maarufu ambao pia hujihusisha na shughuli za soka, amesema kwamba serikali ilipaswa kuwa na subira baada ya kuwapo na taarifa za FIFA kutuma ujumbe wake nchini kwa nia ya kutatua mgogoro uliopo hivi sasa kuhusiana na kuenguliwa kwa baadhi ya watu wanaowania uongozi TFF, wakiwamo Jamal Malinzi anayewania urais na Michael Wambura (makamu wa rais).
Mwanasheria huyo alisema kuwa baada ya serikali kufuta katiba mpya, inamaanisha kwamba sasa mambo mengi yaliyofanyika kwa kufuata marekebisho ya katiba mpya yatakuwa yamevurugika  na baadhi ya wajumbe watapoteza sifa za kuingia kwenye mkutano mkuu.
Aliongeza vilevile kuwa, nafasi kama za Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais wa TFF hazimo katika katiba mpya na badala yake, kuna makamu mmoja tu, tofauti na katiba ya TFF iliyoamrishwa kutumika sasa ya mwaka 2006. Kwa maelekezo ya FIFA, makamu wa rais wa shirikisho (TFF) hawapaswi kuwa wawili bali mmoja.
"Wangesubiri FIFA kuja kutatua tatizo hilo na ndipo serikali ichukua maamuzi yake…  na maana ya FIFA kutuma ujumbe ni kulenga kusuluhisha tatizo," alisema mwanasheria huyo.
Serikali iliamua kufuta katiba ya TFF kutokana na kile ilichoeleza kuwa ni kugundua kwamba marekebisho mapya ya katiba hiyo hayakufuata kanuni na sheria zilizowekwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ambazo ni halali nchini na zimetungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alisema juzi kwamba kabla ya kusajiliwa kwa katiba mpya, TFF ilipaswa kujaza fomu za aina nne tofauti na endapo ingekuwa imekubaliwa, ingejibiwa kwa kupewa fomu namba 11 lakini hatua zote hizo hazikufuatwa.
Kamati ya Utendaji ya TFF itakutana Jumamosi jijini Dar es Salaam kujadili uamuzi huo wa serikali.
Kwa mujibu wa kanuni za FIFA, ni marufuku kwa serikali na mamlaka zake nyingine kuingilia masuala ya soka na hilo likibainika, shirikisho hilo (FIFA) hutoa muda maalum wa kusaka suluhu na ikishindikana, hufungia nchi husika kama ilivyowahi kutokea nchini Kenya.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers