HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

4 June 2009

RAIS KIKWETE AZINDUA MV MAGOGONI

Pichani ni Mv Magogoni ikitia nanga katika kivuko cha feri ambapo kivuko hicho kimezinduliwa leo na rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Mh jakaya mrisho kikwete vilele kivuko hicho kimeigharimu serikali shs bil nane na kinauwezo wa kuchukua abiaria mia nane na zaidi ya ishirini Rais wa Jamhuri ya muungano wa tanzania akushuka kwenye ngani akitoka juu alipokuwa akikagua shuhguri nzima za uendeshaji kivuko hicho Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Jakaya mrisho Kikwete amefungua rasmi kivuko cha Mv magogoni ambacho kitawasaidia wananchi wa kigamboni katika maswala ya usafiri kwani imekuwa kero kutokana na vivuko vilivyopo sasa Mv alina kufanya kazi katika kiwango ambacho hakikidhi matakwa ya wakazi wa kigamboni rais amesema kuwa serikali inafanya kazi kubwa katika kuboresha usafiri wa majini na kuwahaidi wananchi kuwa muda sio mrefu serikali itaanza mchakato wa kujenga daraja ambalo litakuwa la kisasa na kurahisha usafiri kwa wananchi wanaoishi kigamboni pindi wanapotaka kuja Mjini. Nakata Rais wa Jamhuri ya muungano akikata rasmi utepe kuashiria kutumika rasmi kwa kivuko hicho Vilevile mh Kikwete amesema kuwa ule uvumi wa kuwa kigamboni imeuzwa kwa watu maarufu nchini Marekani sio kweli kwani wapo watu ambao hupenda kutunga uongo ambao unawapa faida wanazo zijua wao kwani hamna kitu kama hicho na hakita tokea kwani tuuze kigamboni iliiweje na kwa nini na kwa sababu gani unajua kunawatu ambao hawapendi maendeleo kabisa kwani kwanini tuuze vilevile anakwambia watu wote mtahamishwa sasa mbaya zaidi awaambii mtakapokwenda hamuoni kama ni uongo lakini tatizo kubwa ninyi mnaahamini uongo kuliko ukweli . Jamani Meli hufunguliwa kwa kuvunja Champain ambayo huvunjwa kwa kupigwa kwenye chuma Rais wa jamhuri ya muungano akiwa ameshika chupa ya Champain kulia kwa rais ni waziri wa Miundo Mbinu Shukuru Kawambwa Tupo katika mchakato wa kutengeneza barabara nyingi ambazo zitapunguza adha ya usafiri na msongamano wa magari kwani sasa magari ni mengi lakini sio watu wote ambao wanasafari kuja Mjini lakini kwa sababu njia inapita huko basi lazima wapite. Rais jakaya kikwete akifungua akitambaa kuonyesha kibao kilicho andika kivuko hiki kimezinduliwa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Mh Jakaya kikwete. Rais kikwete alipokuwa akihutubia wakazi kigamboni baada ya kuzindua kivuko cha Mv Magogoni Rais akisalimiana na Baadhi ya viongozi wa wizara ya Miundo Mbinu Kutoka kulia ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam wilam lukuvi na Rais kikwete na waziri kawambwa wakiwa kwenye kivuko kuelekea Kigamboni Ukiangalia kwa mbali utamwona sofia simba akitabasabu bila shaka anafurahia kazi ya bosi wake Rais kikwete akimpa mkono bi sofia simba alipowasiri kigamboni hii leo wakati wa uzinduzi wa Mv Magogoni

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers