Shindano la MAISHA PLUS ambalo limekuwa kivutio hasa kwa watazamaji pia Tanzania Nzima linaanza Tena hivi karibu akizungumzia Shindano hlio mkurugenzi wa Maisha plus Masoud kipanya amesema Usaili umenza leo Tar 22 july kwa mchakato wa kugawa fomu kwa kuzingatia mgawanyo wa kikanda.
Vilevile Mshindi wa maisha plus season 1 ambaye ni Mshiriki Kutoka Zanzibar alisema Kipindi cha maisha Plus ni zaidi ya Maisha kwani unajifunza vitu vingi ikiwemo zaidi ya kuishi na watu mbalimbali wenye tabia tofauti vilevile unapata maisha halisi ya Kijini na Uhalisia wake.Mshindi wa MAISHA PLUS season 1 Abdul Hafidhi alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari katika kumbi ya idara habari maelezo kataika utambulisho wa MAISHA PLUS seson 2
Vilevile kwa upande mwingine Mkurugenzi wa MAISHA PLUS masoud kipanya alielezea kwa upana maana ya kipindi hicho kuwa ni kuelezea kwa upana kwa Jamii uhalizia wa kipindi kile na uwelewa wa kutafakari mambo kiupana zaidi na kujifunza mambo Mengi zaidi kimaisha na maisha ya mtanzania Halisi wa Kijijini.
Zawadi ya Msimu huu ni shilingi Milioni 15 Vigezo vya Msingi vya kuweza Kushiriki ni Umri kati ya miaka ishirini na moja na ishirini na sita Elimu ya Sekondari au iliyo sawa na sekondari chuo cha ufundi na awe na Uraia wa Tanzania viajani wote wana ruhusiwa kushiriki waliooa na kuolewa.
No comments:
Post a Comment