HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

25 April 2010

THE MANARA CAREER

kassim manara akichachafya enzi hizo. yeye ndiye mdogo katika familia ya soka ya manara, ambapo wote walijaaliwa vipaji vya hali ya juu katika uchezaji na hadi sasa hakuna ukoo uliotoa nyota wengi kwa mpigo kama kina manara. Kassim alichezea Yanga kabla ya kuhamia Pan African na baadaye kwenda ughaibuni ambako yuko hii leo ila kwa sasa kastaafu Sunday Manara akikata mbuga. Huyu alipewa jina la Kompyuta kwa uwezo wake. Kumbukumbu zinaonesha yeye ndiye mwanasoka wa kwanza kwenda kucheza soka la kulipwa ughaibuni kwa mafanikio makubwa. Hivi sasa amestaafu na yupo nyumbani Kitwana Manara 'Popat' alianza kama golikipia kabla ya kuamua kuwa mshambuliaji ambapo alitisha sana katika umaliziaji hasa kwa vichwa. Yeye pia amestaafu na anajishughulisha na siasa akiwa diwani na pia mmoja wa washauri kwa shirikisho la soka TFF Kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers