HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

18 March 2013

Hamza Said (Zola) wa yanga Azikwa leo makaburi ya kisutu


Mamia ya wanachama, wapenzi na mashabiki wa soka leo jioni wameshiriki katika safari ya mwisho ya kuusindikiza mwili wa aliyekuwa mfanyakazi wa klabu ya Yanga marehemu Hamza Said (Zola), mazishi yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Mazishi ya Zola yaliongozwa na makamu mwenyekiti wa klabu ya Yanga Clement Sanga, muasisi wa klabu ya Yanga Mzee Jabir Katundu, aliyekuwa mwenyekiti wa Yanga wakili Iman Madega na viongozi wengine mbalimbali waliowahi kuongoza klabu ya Yanga.
Marehemu Zola ambaye alifikwa na umauti jana alfajiri katika makutano ya mitaa ya Rufiji/Congo kwa ajali ya kugongwa na gari, alikua akitokea mitaa ya kariakoo akitembea kuelekea makao makuu ya klabu na ndipo gari hilo lilipomgonga kwa nyuma wakati akitembea kuelekea klabuni.





Uongozi unatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki na wapenzi wa soka nchini kwa kuondokewa na rafiki yetu kipenzi.  
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen 

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers