Shirikisho
la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Leslie Liunda wa
Tanzania kuwa mtathmini wa waamuzi (referee assessor) katika mechi ya
mchujo ya Kombe la Dunia.
Mechi
hiyo ya Kundi B, Kanda ya Afrika kati ya Cape Verde na Equatorial
Guinea itafanyika Juni 8 mwaka huu saa 10.30 jioni kwenye Uwanja wa
Verzea mjini Praia.
Waamuzi
wa mechi hiyo ambao watatoka Angola ni Martins De Carvalho Helder, Dos
Santos Jerson Emiliano, Da Silva Lemos Julio na Muachihuissa Caxala
Antonio. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Diarra Massa Momoye wa
Mauritania.
No comments:
Post a Comment