Mwamuzi kutoka Italia Nicola Rizzoli amaetangazwa kuchezesha mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya baina ya Borussia Dortmund dhidi ya Bayern
Munich mchezo utakao pigwa katika uwanja Wembley siku ya jumamosi .Mwamuzi huyo mwenye miaka 41- amekuwa mwamuzi wa kimataifa tangu mwaka 2007.
alichezesha mechi ya kwanza ya fainali ya ligi ya ulaya mwaka 2010
iliyochezwa uwanja wa Hamburg, ambapo Atlético de Madrid iliifunga Fulham FC 2-1 katika muda wa nyongeza ,na amechezesha mechi tatu katika michuano ya ulaya EURO 2012. kiujumla , Rizzoli
amechezesha na kuhusika katika mechi 26 za ligi ya mabingwa barani ulaya ,nne kati ya mechi hizo ni za msimu huu ikiwemo ya mkondo wa pili wa hatua ya 16 kati ya Málaga CF na FC
Porto.
Mwamuzi huyo atasaidiwa na wataliano wenzake Renato Faverani na Andrea Stefani. na mwamuzi wa nne atakuwa Damir Skomina kutoka Slovenia na wamuuzi wengine wa akiba ni , Gianluca Rocchi na Paolo Tagliavento,wote kutoka italia . wamuuzi ambao watakuwa katika benchi kama mabo yataaribika ni – Gianluca Cariolato –
ambao wanamaliza timu ya waamuzi wa mchezo huo.
No comments:
Post a Comment