Manchester United imesisitiza kuwa mshambuliaji na kiuongo wa timu hiyo Wayne Rooney hauzwi baada ya yeye mwenyewe kuomba kuondoka kwa mara ya pili katika viunga vya Trafford mchezaji huyo mwenye miaka 27-ambaye ni mchezaji wa zamani wa Everton alimwambia Sir
Alex Ferguson majuma mawili yaliyopita kuwa angependa kuondoka baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka tisa Msemaji wa uinted
amesema : "Wayne Rooney hauzwi " Taarifa hizi zinakuja baada ya kocha wa timu hiyo kutangaza kujiuzulu mwishoni mwa msimu huu
Rooney kama atasaria united ataungana na kocha wake wa zamani David Moyes, ambaye atatangazwa kama mrithi wa Ferguson leo badae Roney akiwa na 18, aliuzwa na Moyes akitokea katika klabu yake
Everton August 2004 kwa gharama ya £27m. na amekwisha funga magoli 197 katika mechi 402 akiwa na manchester united ,Na ameshinda mataji matano ya ligi ya premier, na mawili ya Carling cup kombe moja la ligi ya mabingwa barani ulaya na msimu huu amefunga magoli 16 katika mechi 37 kati ya magoli hayo kumi na mbili kwenye ligi kuu ambapo wametwaa ubingwa hivi karibuni
likiwa ni taji la 20 kwa klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment