Mechi
namba 149 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Mgambo Shooting
iliyochezwa juzi (Mei 8 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
na kumalizika kwa Simba kushinda bao 1-0 imeingiza sh. 16,651,000.
Watazamaji
3,006 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa
sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata
mgawo wa sh. 3,226,125 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT)
iliyolipwa ni sh. 2,539,983.05.
Mgawo
mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 1,640,402.54,
tiketi sh. 3,175,000, gharama za mechi sh. 984,241.53, Kamati ya Ligi
sh. 984,241.53, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
492,120.76 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh.
382,760.60.
No comments:
Post a Comment