HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

25 February 2014

LESENI YA OKWI HII HAPA !!!



Klabu ya soka yanga ya Dar Es salaam leo imeonyesha  leseni inayomruhusu mchezaji wake mpya Emanuel  Arnod Okwi kuchezea klabu hiyo katika michuano ya kimataifa baada ya kutokea mikanganyiko ya muda mrefu kwa kutokuelewana baina ya wadau wa soka mawakala ,vyombo vya habari, fifa na shirkisho la soka afrika caf na klabu ya Etoile du Sahel .

Msemaji wa klabu ya yanga Baraka kizuguto ameonyesha leseni hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhsu maandalizi ya timu hiyo dhidi ya timu soka ya Al AHLY  katika michuano ya klabu bingwa barani afrika mchezo utakao chezwa siku ya jumamosi katika uwanja wa taifa jiji Dar Es salaam mzunguko wa pili kuwani ubingwa wa afrika ambapo al ahly ni Bingwa mtetezi.

Emanuel alikuwa akiitumia klabu ya simba kabla ya kuuzwa kwenda katika klabu ya Etoile Du sahel ya Tunisia ambapo mapaka leo simba haija pata pesa zake katika hari ambayo bado haijafamika mpaka leo haijajulikana kama kandarasi ya mchezaji huyo imekwisha au bado lakini kulilipotiwa kuwa aliwahi kuishtaki klabu hiyo kuwa haijampatia mshahara wa miezi mitatu na hivyo kuvunjika rasmi mkataba wake nahii ni kwa mujibu wa wakala wa mchezaji huyo na Emanuel okwi mwenyewe.

Lakini kwa upande mwingine Klabu ya sahel ilimshtaki Okwi fifa kuwa ni mtoro baada ya kushindwa kurudi katika klabu ya sahel wakati alipokwenda kuitumkia timu ya taifa ya uganda katika mmichano ya kombe la dunia , kitendo kinachosemekana mpaka leo hakijafanyika kwa okwi.
Lakini shirikisho la soka la kandanda la Tanzania liliwahi kuuliza kuhusu mustakbari wa mchezaji huyo kuchezea klabu ya Yanga na kwa mujibu wa barau hiyo ilisema hivi “Jukumu la kumuidhinisha mchezaji kucheza katika timu ya nchi husika ni jukumu la chama cha soka cha nchi husika na kama mmefuata sheria inavyotakiwa haina tatizo “
Lakini katika hari isikuwa ya kutegemewa Mwenyekiti wa klabu ya soka ya simba  alikuwa na nyaraka za siri za ambazo anadai alitumiwa na  Sahel ya Tunisia zikionyesha kuwa Okwii ni mali ya sahel .

Lakini je nini kitatokea katika sinema hii ya sakata la Emanuel okwi ambalo Etoile Du sahel na Shirkisho la soka Afrika Caf ambao ndio wametoa leseni huku Al AHLY wakionekana kanakwamba hawajui kinachoendelea ni jambo la kusubiri kisheria kwani zipo mechi nyingi ambazo matokea yamewahi kutenguliwa kutokana blanda za kuchezesha wachezaji isivyo utaratibu.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers