HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

8 March 2014

JE NI KWELI WACHEZAJI WA KITANZANIA HAWAFUNDISHIKI ???



Hivi karibuni nilipata kuskia kocha wa klabu moja hapa nchini akisema wachezaji wa Tanzania hawafundishki  watu walio wengi walimtukana kocha Yule na kusema kuwa amewadharau wachezaji wa kitanzania hawafundishiki mimi sasa nanyanyua kinywa na ninasema ndio  hawafundishi nina amini hawakumuelewa mkufunzi huyu napengine sio wachezaji wa kitanzania hata raia ambao sio wachezaji nini maana ya kutofundishika ?



Maana yake kutofuata maagizo ya mwalimu na kufanya yale ambao hukupewa hii ndio maana ya kutofundishika ndio maana Hata klabu mbili za simba na yanga kubadili makocha kila siku iendayo kwa mungu hii ndio maana ya kutofundishika  wengi walikasilika hata wadau mbalimbali wa soka wakisema kocha Yule kawakosea heshima wachezaji wa kitanzania Binafsi yangu ninasema wala hakuwakosea heshima alisema ukweli tatizo ni kutokukubali ukweli .



Mara kadhaa Tanzania imeshindwa kufanya vizuri sio klabu wala timu ya taifa hata wakati makocha wa kigeni wamekuwa wa kibadili wachezaji mara kwa mara hii inaonyesha kuwa hata makocha wamekuwa wakishindwa kupata safu nzuri ya wachezaji kwa sababu ya uelewa mdogo wa wachezaji wa kitanzania na timu chache sana ambazo huwa zinaweza kuka na wakufunzi kwa muda mrefu na timu zote ambazo zimekuwa zikibadili makocha kila kukicha hii ina maana ya kuwa hawafundishi kwani huwezi kubadili makocha kama unafanikiwa haina sababu.

kocha wa kigeni toka ulaya ambaye amewahi kukaa kwenye klabu kwa zaidi ya miaka mitano hakuna .



Na kutokana malezi hafifu ya watoto wa kitanzania ni vigumu sana kupata mchezaji anayeweza kufundishika ni vigumu kwani katika mazingira ya kitanzania baadhi ya wachezaji wa kitanzania hawajui hata kiingereza kwani Kiswahili tun kinawapa shida na matokea yake hushia kuzungumza Kiswahili cha mtaani na walio wengi hawakukaa darasani kukaa na mwalimu anae zungumza  kingereza ni ndoto kuelewa hakika na kubaliana na mkufunzi huyu kwani uelewa wao hata katika masomo ya shuleni ni mdogo ndio maan sifuri ni nyingi darasa saba kidato cha nne hadi kidato cha sita na walio wengi hujaribu hata kufoji matokeo ili waende chuo kikuu sasa tukiambiwa hatufundishiki mtakataaa .



Tunaweza kuweka  vigezo vya kutafuta kocha lakini lazima tujiulize je tuna aina ya wachezaji wa mpira wa miguu wanaoweza kuchezeshwa na kocha mpya je itawezekana vipi jambo la msingi ambalo watanzania wanatakiwa kuelewa mfumo mzima wa kielimu Tanzania auwiani na  wanafunzi kila waziri wa elimu anayekuja kuongoza wizara anakuja na mtazamo mpya je mnafikiri ni rahisi kuona soka yakufundishwa kwa tanzania kila siku tunalia jinsi ya kutafuta wachezaji  jambo ambalo limekuwa ndoto kushiriki michuano ya vijana na tumeishia kudanganya umri .



sasa maana ya kutofundishika ni kudanganya umri kwa sababu kama umeshindwa kugundua umri sahihi au kupindisha sheria kimakusudi huko ni kutofundishika jamani .

Watanzania wenzangu lazima tutafakari kabla ya kuanza kutuhumu mtu anapotoa kauli yake ya watu kutofundishika .



No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers