HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

23 March 2014

WAAMUZI WA TANZANIA NA SHUTUMA ZA KUTOA HAKI UWANJANI NI RUSHWA AU WEREDI?




Jambo la kwanza la kujiuliza kwanini  waamuzi wetu wa Tanzania hawacheshezi fainali za mataifa ya afrika ? au kwanini waamuzi wetu hawachezeshi mechi kubwa  za vilabu vyetu vya afrika   hili ni swari ambalo kwa mtanzania yoyote Yule anaweza kukupa jibu sahihi kwa anavyofikiri lakini kikubwa na cha maana zaidi ambacho watu wanatakiwa kufahamu na kuhitaji kuelewa ni kwanini haya yote yanafanyika katika nchi yetu ambayo kila kukicha timu zina lalamikia waaamuzi na kusema hawachezeshi vizuri.

Jambo la kwanza na kuu kuliko yote je waamuzi wetu wanajua wanacho kifanya uwanjani ? lakini la pekee na kubwa zaidi ni kuwa kwanini waamuzi wetu hawachezeshi mara kwa mra katika mechi za klabu hasa katika hatua ya Robo fainali ya klabu bingwa afrika au kombe la shirikisho au mashindano ya Chan hii ina maana kubwa kwetu kuwa waamuzi bado Uwezo wao upo katika kiwango cha chini lakini ni waamuzi hawa 
ambao wanalalamikiwa kila kukicha kupokea Rushwa za Hari ya juu lakini inawezekana likawa linasababishwa na ubora finyu wa klabu zetu na ligi yetu ya Tanzania kuwa hatupo katika  ubora unaostahiri .
Kwa kiasi kikubwa bara la afrika limegawanyika sana katika ubora wa soka na hata waamuzi hutoka kwa ubora wa kanda ukitazama vizuri Nchi za afrika Magharibi na kaskazini mwa afrika ndizo nchi zenye ubora zaidi kisoka na ndizo zinatoa timu mara kwa mara katika fainali za afrika na kombe la Dunia kwa hiyo kutokana na ubora wa soka ndipo hata uwezo wa  waamuzi unaopatikana na kuongezeka kwa hari ya juu  na hii inasababishwa na mikiki ya ligi na utimamu wa mwili, leo hii Tanzania ina makamishna watatu mmoja Zanzibar na wawili bara akiwemo mwanamke mmoja.

Sasa kwa hatua tuliyopo sasa shirikisho la soka la Tanzania lina kazi kubwa ya kuhakikisha ya kuwa inafanya kazi ya ziada kutazama ni kwa jinsi gani tunaweza kutengeneza Safu nzuri ya waamuzi katika soka ya Tanzania Tff ilipiga mkwara kuwa timu yoyote itakayo lalama kuhusu waamuzi basi itachukuliwa hatua za kisheria kauli hii ni ya Umwamba zaidi na ya utawala wa mabavu kwa sababu kamati inayotazama waamuzi katika shirikisho la soka la Afrika kila mwaka inachagua kwa kudonoa donoa waamuzi kutoka Tanzania hii ina maana CAF imeshajua kuwa Tanzania hakuna waamuzi wanaoweza kutafsiri sheria kiusahihi kwa asilimia Angalau sitini lakini hili lina shaka ndani yake wachezaji wengi wa watanzania uwezo wa kutafsiri sheria za soka ni Mdogo sana ndio maana wanashindwa kucheza ulaya.

Lakini tunahaja ya kulitazama upya jopo la waamuzi la Tanzania ndani ya shirikisho la Soka kwa sababu kubwa ni kwamba nani anayetoa tathimini ya Waamuzi hawa kwanini kila mwaka tunachemsha huwa tunaskia makocha tu wanapata kwenda nje kwa ajiri ya mafunzo lakini waamuzi wetu sidhani kama wanakwenda mafunzo ya uamuzi wa mchezo wa mpira wa miguu kwa sababu sheria zinabadilika kila uchao kwa kutazama katika mitandao wakati Uefa wakiboresha Sekta ya waamuzi kwa kuweka Waamuzi watano kiwanjani .Leo Tanzania bado tupo katika hatua  ile ya kuweka waamuzi watatu.

Je kwa mambo kama haya unadhani makocha,wachezaji,na waamuzi wenyewe ambao nao wanashindwa kutafsiri unadhani kuna kitu ambacho tunaweza kufanikiwa  kupata mwamuzi hii ina maana kuwa tunahitaji kuwa na upana mkubwa zaidi wa kutanua wigo wa Elimu hasa wa kimataifa kwa waamuzi wa soka la Tanzania bila hivyo tutakuwa tunalamikia waamuzi kila siku kwani inawezekana kuwa kuna mambo ya kina ya kuzingatia katika sekta hii ya utoaji wa haki kiwanjani.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers