HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

1 March 2014

WACHEZAJI WA TANZANIA HAWAJUI ABCD ZA SOKA




Moja kati ya mambo ya msingi ambayo  watanzania wengi wanataka katika soka ya Tanzania  ni ushindi bila kujari unapatikana vp ? Mara nyingi huwa tunasingizia kuwa hatuna maandalizi ya kutosha ya kupambana  na timu pinzani je tunahijati maandalizi ya aina gani ili tuweze kufanikiwa angalau kucheza michuano ya kimataifa.

Katika kulitazama hili nimekaa na baadhi ya makocha wa Tanzania ili kuweza kujua tatizo nini ni ? hasa kiasi cha Tanzania kushindwa kufnya vizuri sio katika soka tu bari katika michezo yote Tanzania .
Moja kati ya majibu ya kimsingi ambayo  nimeyapata  katika tafiti zangu nilizo fanya, kuu kuliko yote ni kuwa wachezaji wa Tanzania hawajui ABCD za mpira wa miguu kiasi ambacho wachezaji wengi wa kitanzania wanashindwa hata kufanya majaribio nje ya nchi.

Ni vigumu mmno kufanikiwa hata kama tukaleta kocha kutoka Ujerumani au uholanzi naam wengi wetu tumekuwa tukiweka siasa ya kuwa hakuna kisichowezekana  katika mpira wa miguu  lakini ukitazama kiuhalisia wachezaji wa kitanzania na makocha wetu wa leo hawajui soka la kiufundi kabisa na kuna makocha wa chache ambao wanajua kufundisha soka la kiufundi lakini wamekuwa hawapewi nafasi kwani nabii siku zote huwa hakubaliki kwao
.
Kwa hari ilivyo sasa ni lazima tupeleke makocha wetu nje ,wakasome na waje kufundisha soka ndani ya nchi yetu na wakatembee katika mashule ya ili waweze kutoa elimu ya soka katika shule zao bila kufanya hivyo tutakuwa tunampigia mbuzi gitaa kila mwaka .

Lakini poulsen anaondoka huku akisema kuwa wachezaji wa kitanzania sio professional wa kucheza mpira wa miguu kwani hawakuandaliwa kufanya hivyo ni wavivu wa kula na vile vile wanacheza mechi wakiwa wamefunga  je unadhani ni rahisi kucheza soka kwa mchezaji ambaye anacheza soka ya ridhaa professional ligi ya Tanzania ni professional lakini wachezaji hawana matendo ya kiprofesional 

Bila kuelewa ABCD za mpira wa miguu itamchukua mchezaji mmoja wa kiatanzania Miaka mia moja na themanini kuwa sawa na wachezaji wanaocheza ligi daraja la nne ulaya sababu hawajui ABCD za mpira miguu na  najua unaaniuliza zimnapatikana wapi  ABCD  za soka timu za Tanzania zinatakiwa kuwa shule za soka ambazo zitakuwa maalum mtoto afundishwe akiwa mdogo na Elimu ya dunia waijue wakiwa tangu watoto . 

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers