HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

10 April 2014

MAN U YAGONGWA NA BMW,BARCA YAONJA LADHA YA VICENTE CALDERON


Manchester United imechemka kutinga hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya baada ya kufungwa na  Bayern Munich huku wakiendeleza ushindi katika katika Record baina yao .

United inayoongozwa na David Moyes's ilitoka suluhu na  Bayern ya  1-1 katika Dimba la Old Trafford katika mzunguko wa kwanza na walianza vizuri baada ya  Patrice Evra kufunga la uongozi japo bao hilo lililudumu kwa dakika moja katika kipindi cha pili. 

  Baada ya Mario Mandzukic kusawazisha bao hilo kwa kichwa na kabla  ya  Thomas Muller's ajamalizia krosi iliyopigwa na Ribery kupachika bao la pili . 

Alikuwa Arjen Robben tena aliyekata chenga  na kupiga shuti lilimparaza Vidic na kumpoteza maboya De gea na kufuga bao la tatu na matokeo kusomeka  4-2 kwa jumla .


 Koke scores for Atletico Madrid v Barcelona

Atletico Madrid imeitoa  Barcelona  katika ligi ya mabingwa baada ya Koke kufunga goli la mapaema katika mzunguko wa pili katika dimba la  Vicente Calderon.
Kichwa kilichopigwa na kiungo huyo na kuipa timu yake uongozi wa goli mbili moja kwa ushindi wa jumla .
Madrid walipiga mashuti matatu ndani ya dakika ishirini.
Gabi alipoteza nafasi ambayo ingemfanya kumaliza mechi mapema , Huku  Neymar  akijaribu kusawazisha na  kwa kuruka kichwa cha kuchupa kwa chini lakini haikusaidia .

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers