HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

3 April 2014

SAIDO BERAHINO KUMSHITAKI MORRISON MAHAKAMANI !


Mchezaji na Mshambuliaji  West Bromwich Albion  Saido Berahino yupo katika harakati ya Kutumia Haki yake kumshtaki mchezaji mwenzake wa Timu hiyo  James Morrison, Hii ni kwa Mujibu wa mwanasheria wa mchezaji .
Berahino anasema kuwa walikuwa wakijibiza na mchezaji mwenzake  Morrison katika mechi ya ligi ya Uingereza siku ya Jumamosi katika mchezo ulioisha kwa suluhu ya Mabao matatu kwa matatu   3-3  Dhidi  Cardiff City.

Wachezaji hao walizozana katika vyumba vya kubadilishia Nguo   Baada ya  Morrison kuwa mkali kwa  baada ya mchezaji kukataa kuomba radhi kwa wachezaji wenzake baada ya kupoteza mpira katika dakika za mwisho na kuipa nafasi  Cardiff's kusawazisha katika dakika za Nyongeza  .

Taarifa zinasema kuwa siku ya Jumamtano mchezaji huyo wa timu ya taifa ya uingereza chini ya miaka -21  alikuwa akitarajia kuchukua hatua za kisheria kwa kiungo huyo wa Uskochi  Morrison.
 Ashley Wooton, Ambaye kwa sasa ni mwanasheria wa maalumu wa  Thomas Eggar LLP, anaamini kuwa Berahino anaweza kuwa na hoja za kufungua Madai hayo .

Anasema : "James Morrison anaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu Dhidi ya Klabu yake kama atakubali makosa  au kama atatiwa hatiani . Berahino anaweza fungua mashitaka Dhidi ya  Morrison kwa Tabia mbaya na isiyo na ulazima  .


No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers