HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

11 July 2014

ADEN RAGE AKABIDHI SIMBA AMPA MZIGO MKUBWA AVEVA .

Rais aliyemaliza muda wake Simba Ismail Aden Rage akabidhi nyaraka na mali ya klabu kwa Rais mpya wa klabu hiyo Evance Aveva
Aliyekuwa mwenyekiti wa klabu ya Simba Ismail Aden Rage hii leo amakabidhi ofisi kwa uongozi mpya wa klabu hiyo ambao unaongozwa na Evance Elieza Aveva mara baada ya kukamilika kwa zoezi la uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwezi uliopita.
Ismail Aden Rage amefanya makabidhiano hayo ya ofisi kwenye makao makuu ya klabu ya Simba ambapo amekabidhi nyaraka mbalimbali za kiutendaji wa klabu hiyo kongwe hapa nchini.
Hata hivyo rage ameushauri uongozi wa Evance Aveva kufuata taratibu ambazo alizitumia wakati wa uongozi wake wa kipindi cha miaka minne hususana katika suala la vyanzo vya fedha.
Kitu kingine ambacho Rage amekigusia ni kumtaka Rais wa klabu ya Simba Evance Aveva kutatua kwa kutumia busara suala la wanachama wa klabu hiyo waliokwenda mahakani kwa lengo la kuzuia uchaguzi.
Katika hali ya kushangaza Ismail Aden rage akazungumzia na kukabidhi nyaraka zinazoonyesha uhamisho wa mshambuliaji Emmenuel Okwi ambae aliuzwa na klabu ya Simba huko ndhini Tunisia kwenye klabu ya Etue Du Sahel.
Baada ya kukabidhiwa nyaraka za klabu ya simba Rais mpya Evance Aveva alimshukuru Ismail Aden Rage kwa niaba ya kamati yake ya utandaji huku akimtaka kutojiweka mbali mba wao kutokana na kuona bado kuna hitajiko la nguvu zake ndani ya klabu hiyo ya Msimbazi.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers