HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

24 August 2014

REAL MADRID YAUA TAIFA YAIPIGA TANZANIA 11 (3-1) NI RUBEN DELA RED

Gwiji la soka la Real Madrid Ruben Dela Red akifunga penati na kuifungia Timu hiyo bao la Tatu katika mchezo wa Bonanza lilokutanisha kati ya wachezaji wa Real Madrid na Tanzania 11

Ruben Dela red ameifanyia Maangamizi Tanzania 11 iliyokuwa ikifundishwa na Charlse Boniface Mkwasa pamoja na Jamhuri kiwelo katika mchezo kirafiki uliokutanisha wachezaji wa zamani wa Real madrid na Tanzania 11 .

Real ndio waliokuwa wa kwanza kupata Goli katika Dakika ya Kumi ya Mchezo pale Christian Karembeu alipoanzisha mashambulizi hadi kwa Luis Figo na baadae kumkuta Ruben Dela Red na kumchambua Mlinda Mlango Mohamed Mwameja .
lakini katika Dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza Tanzania 11 ilisawazisha goli baada ya Real Madrid kujifunga katika harakati za kuokoa Robrto Rogers alijifunga mwenyewe baada ya kona kuchongwa na Kalima ngonga Ongara mpaka nusu ya kwanza ya mchezo Tanzania eleve moja Real madrid moja.
Kipindi cha pili Ruben Dela Red alifunga bao la pili  katika dakika ya Themanini ya mchezo na baadae kumaliza kwa kufunga bao la tatu kwa njia ya Penati .
Moja kati ya wachezaji waliokuwepo katika timu ya Tanzania 11 ni Mohamed mwameja,keneth mkapa ,Boniface pawasa,Nasoro Mwinyi Bwanga,peter Manyika,Lunyamila,Dua said,Nsajigwa Shadrack,Athuman Abdallah China ,mwanamtwa kiwelo, 
wakati kwa real madrid wachezaji wanaojulikana zaidi kwa upande wao alikuwepo fabio canavaro,Christian Karembeu ,Luis Figo,Fernando Sanche.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers