HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

28 November 2012

LUIZ ADRAIANO AFUNGIWA MECHI MOJA KWA KTOONYESHA UUNGWANA KIWANJA

Mshambuliaji wa   Timu ya soka ya  Shakhtar Donetsk  Luiz Adriano amefungiwa mechi moja katika michuano ya ligi ya mabingwa ulaya iliyochezwa jumaane iliyopita mara baada ya kushindwa kuonyesha uanamichezo,  baada ya kufunga goli ambalo halikuwa la kiushindani Dhidi ya  Nordsjaelland.

Kamati ya Nidhamu ya UEFA imemkuta na hatia  MBrazil huyo baada ya kujikuta akizua mijadala na kuvunja taratibu za soka katika mchezo uliochezwa huko  Denmark wiki iliyopita

"Mchezaji huyo wa  Shakhtar amepewa maagizo na 
UEFA  ya kufanya shughuri za kijamiii za mpira wa miguu  .

Luiz Adriano alivunja sheria ya uanamichezo mara baada mpira kusimamishwa kupisha mchezaji wa timu pinzani kupata matibabu  .
Baada ya Mpira kuanzishwa kwa  kundundishwa  Adriano alikimbiza mpira na kumpiga chenga beki  wa Nordsjaelland na baadae kumpiga chenga kipa na kufunga goli ambapo sasa atatumikia adhabu dhidi ya Juventus  December 5, japokuwa mabingwa hao wa  Ukrain wameshafuzu hatua inayofuata baada ya kuifunga  Nordsjaelland 5-2.



UMOJA WA CHAMA CHA WAAMUZI WAKUBALI RADHI YA CHELSEA 


Chama cha Waamuzi uingereza  wameridhia  kauli ya klabu ya chelsea kujutia malalamiko yake ya dhidi ya ubaguzi wa rangi yaliyotolewa dhidi mwamuzi  Mark Clattenburg 'kuwa wamekubali makosa '.

Katika Taarifa ya majumuisho iliyotolewa na Bodi ya waamuzi wanaochezesha michezo ya  kulipwa kisheria   (PGMOL)  ambao huchezesha ligi ya uingereza na  ,Ligi ya mbaingwa ulaya  wamejutia kutokuwa na ushahidi wa kutosha katika malalamiko yao waliyoyatoa  28 October wakimtuhumu mwamuzi kwa ubaguzi wa wa Rangi .

Wiki iliyopita ,Chama cha soka cha uingereza kilitoa taarifa kuwa hakuna kesi ya kujibu Dhidi ya   Clattenburg,

ambaye ana miaka  37, kuwa alimtukana mchezaji wa kimataifa wa nigeria na kiungo wa cheslea  John Obi Mikel ambapo  Chelsea ilifungwa mabao matatu  3-2 dhidi ya Manchester United.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers