HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

21 December 2012

MALAGA KUTOTETEA UBINGWA WA ULAYA MWAKANI !



Timu ya soka ya  Malaga imefungiwa kwa mmoja kutokushiriki ligi ya mabingwa barani ulaya kwa msimu unaokuja baada ya kushindwa kulipa mishahara na kodi za wachezaji kwa wakati. 

UEFA imesema kuwa Raia wa Qatari-ambaye ndiye anae miliki timu hiyo ameambiwa atafungiwa zaidi miaka minne kama
watashindwa kulipa madeni hayo ,mpaka mwezi  March 31 ambayo ndio siku ya mwisho aliyowekewa kulipa madeni hayo  anatakiwa kulipa dola za kimarekani  $11.6 zikiwa ni mishahara ya wachezaji .

UEFA  imetangaza hayo jana baaada ya timu hiyo kupangwa kucheza na Fc Porto katika hatua ya mtoano kumi na sita bora ya ligi ya mabingwa barani ulaya  timu hiyo haitaruhuisiwa kucheza ligi ya mabingwa au Europa ligi kama watafuzu msimu ujao  .

UEFA's imeipiga faini klabu hiyo ya  Malaga Dola $396,000.Timu hiyo inaruhusiwa kukata rufaa katika mahakama ya usuluhishi wa michezo CAS  

Malaga Inatarajiwa kupata jumla ya dola  a $33 million kutoka uefa ikiwa kama zawadi katika malipo ya runinga baada ya kushiriki ligi ya mabingwa bara ulaya 

Malaga imefuzu kwa mara ya kwanza kucheza michuano hii mikubwa baada ya kumaliza wa nne katika ligi ya uispania msimu uliopita 
Klabu hii ilipata nguvu baada ya kuchukuliwa na mwekezaji kutoka Qatar  Sheik Abdullah Bin Nasser Al-Thani


Klabu nyingine ambazo zimekumbwa na adhabu hiyo ni  - Bucharest clubs Dinamo  Rapid,  Partizan Belgrade kutoka serbia ,  Hajduk Split , Osijek ya  Croatia - ambazo zimefungiwa kwa miaka mitatu  zaidi kama watashindwa kulipa faini hiyo hadi mwezi march 31 .

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers