HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

22 February 2013

Waziri ataka michezo ipewe nafasi shuleni


 

 Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Kassim Majaliwa, amewataka wakuu wa shule za msingi na sekondari nchini kuanzisha program za michezo shuleni na kuzisimamia ipasavyo.

Majaliwa aliyasema hayo wakati wa siku ya mwisho ya ziara yake mkoani Singida wakati alipokutana na watendaji wa sekta ya elimu kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Waziri Majaliwa alikumbusha kuwa, serikali imesharudisha michezo shuleni na hivyo programu za michezo zinapaswa kupewa nafasi huku pia akizitaka halmashauri za wilaya, miji, manispaa na majiji kuipa michezo kipaumbele kwa nia ya kuibua vipaji vipya kwa manufaa ya klabu na timu za taifa za michezo mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers