Michuano ya mpira wa kikapu ya Ali Yussuf Thabit Kombo Inaanza kesho kisiwani Pemba huku timu kumi na mbili 12 zikitarajiwa kushiriki .
Aidha mashindano hayo yatajumuisha jinsia zote mbili zitashiriki pamoja na bingwa mtetezi Tornado hii ni kwa mujibu wa chama cha mpira wa kikapu Zanzibar, BAZA.
katika hari isiyotegemewa aliyewahi Rais wa ZFA Amani Ibrahim Makungu anatarajiwa kuwa mgeni wa heshima katika ufunguzi wa Mashindano hayo
Mwenyekiti wa BAZA Charles Augustino Lubega amesema kuwa maandalizi yamefikia hatua nzuri kwa sasa na wameyaandaa kwa ajiri ya kutangaza visiwa hivyo vya Zanzibar .
wamechaguwa kisiwa cha pemba ili kusaidia ukuaji wa mchezo wa kikapu kisiwana humo ..
Kila timu itakayoshinda katika kila jinsia itapata shilingi lakini tatu 300,000/-, Na pea moja ya jezi na mipira mi tatu .
Huku washindi wa pili watapata 200,000/- , na mipira miwili .huku mshindi wa tatu atapata shilingi 100,000/-,na pea moja ya jezi na mpira mmoja .
No comments:
Post a Comment