HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

9 March 2013

KIKWETE :HUU NDIO MZIZI WA FITNA KATIKA MAENDELEO YA SOKA NA MAENDELEO YA MICHEZO TANZANIA

http://www.bongocelebrity.com/wp-content/uploads/2009/11/World-Cup-1024x935.jpg
Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania JK


Lazima tutazame vilabu vyetu hapa Nchini Vinaongozwa zaje, wengi wetu tunafahamu kuwa  haviongozwi vizuri huo ndio mzizi wa fitina bila kulitazama hilo hatutaweza kusonga mbele hadi mwisho wa Dunia   

Leo nimeona tutazame kwa undani kidogo  kuhusu matatizo yanayofanya Nchi yetu ya Tanzania kushindwa kufanya vizuri kimataifa ! wengi wetu huwa tuna majibu rahisi katika maswali magumu  lakini hapa lazima tutafakari kwa kina tunashidwa kwa kiasi gani ama nini kinatufanya  tushindwe kufanikiwa katika Nyanja ya kimataifa ?

Moja kati ya mambo yanayoharibu soka au michezo kwa taifa la Tanzania Ni mfumo wa uendeshaji wa michezo yenyewe, tuanze na vilabu vya soka ambapo kwa nchi kama ya Tanzania kama hujazungumzia simba na yanga bado haujazungumzia soka la Tanzania hapa nadiliki kusema hawa ndio wachawi wanaoharibu soka lote la Tanzania.

Tangu Rais mwinyi aliposhuhudia simba inafungwa nyumbani na stela Abidjan ya ivory coast aliibatiza jina la kichwa cha mwendawazimu  hii sio tu kiwanjani kuanzia klabu husika mpaka na uongozi mzima .

Kwa Takriban muongo mmoja uliopita klabu za simba na yanga zimekuwa kwenye migogoro isiyokwisha tena chaa ajabu imekuwa ikija kwa kupishana pishana leo simba kesho yanga swali la kujiuliza wanaoongoza vilabu hivi wanajua hata ABC ya uongozi kwanini imekuwa kero kila kukicha simba na yanga na vilabu hivi vimekuwa vikiambukiza na timu nyingine katika za ligi hiyo ambavyo ni vya kiraia kwa muongo huu mmoja,
 sikuwahi kusikia Timu inayomilikiwa na jeshi kuwa na mgogoro pengine inatokana na aina ya uongozi walionao .

Klabu za simba na yanga hutegemea sana wachama ambao swala kufungwa huwa halipo kabisa katika akilizao kana kwamba wao wameandikiwa kushinda tu au kutoa suluhu kitu ambacho sio kweli kwani hata Brazil hufungwa kwani ndio timu pekee iliyotwaa ubingwa wa dunia mara nyingi zaidi .

Pengine ifike mahali kubadilisha mfumo wa aina ya wanachama kwani aina ya mfumo  wanachama wa simba na yanga ninamashaka nao lakini inawezekana wanalipa mamiliano ya shilingi ndio maana wanaskia uchungu sana timu inapofungwa lakini kwa kumbukumbu nilizonazo pesa wanayolipa haizidi hazidi hata shilingi elfu mbili mia tano.

Ni mara chache sana kusikia vilabu vya ulaya kuwa na migogoro hata sehemu za afrika kama afrika kaskazini, kusini mwa afrika na maghalibi lakini kwa Tanzania haupiti Mwaka utaskia kelele kibaya zaidi unaweza kuchaguliwa kwa kura nyingi lakini mwisho wa siku hukaonekana hauna maana hata kidogo hizo ndizo simba na yanga .

Ukiachia simba na yanga vilabu vingi vianyoshiriki ligi Tanzania au hata visivyoshiriki ligi Tanzania vina kabiliwa na tatizo kubwa la kiuchumi ukitazama kiuzamini wazamini wengi hukimbilia kuvizamini vilabu hivyo hivyo ambazo haviishi migogoro je kuna uwezekano wa pesa za wazamini hawa zikawa zinaanzisha migogoro vilabu hujazwa mapesa na kuwa na nguvu kiuchumi na hupambana na timu ambazo wakati mwingine nauli za kusafiria havina kabisa .

Tangu viwanda kadhaa vife au kushindwa kujiendesha timu zao ushindani wa soka na michezo mingine umekufa kabisa mfano mzuri kiwanda cha ushirika cha mkoani Kilimanjaro kilikuwa kikimiliki timu ya ushilika ya moshi.
  Lakini tangu kiwanda kife na timu nayo imekufa viwanda vingi vimeshindwa kuendesha timu kama sigara ambao walikuwa na timu ambayo iliwahi kushiliki hata mashindano ya kimataifa , zipo timu nyingi za mashilika ya umma ambayo ya leo mashilika husika na timu zake zimekufa lakini kikubwa kinachooneka ni aina ya uongozi wa viwanda na vilabu husika kushindwa kuendesha timu.

Jambo la msingi apa vilabu vya soka na vyama vimeshindwa kupata viongozi sahihi  wa kuongoza taasisi hivi na sio vilabu hata serikali nayo imeshindwa  ,kwa mfano simba na Yanga zimekuwa zikitumia mamilioni ya shilingi kusajiri wachezaji walioshindikana nchini mwao ambao wachezaji hao wameshindwa  kuzisaidi simba hata kufika robo fainali ya klabu bingwa afrika kama sio kombe la  shirikisho.

 Mapesa wanayotumia kununua wachezaji kwa muongo mmoja yangeweza kabisa kutengeneza mradi wa ukuzaji wa vipaji vya watoto lakini yote haya yanasababishwa na mifumo iliyoooza ambayo hata Mbwa hawezi kunusa Rais kikwete aliwahi kusema katika ziara ya kombe la dunia kuwa
 “Lazima tutazame vilabu vyetu hapa nchini Vinaongozwa zaje wengi wetu tunafahamu kuwa  haviongozwi vizuri huo ndio mzizi wa fitina bila kulitazama hilo hatutaweza kusonga mbele hadi mwisho wa Dunia “
 Naam ipo haja ya kuutafakari usemi huu lazima tutazame mifumo ya uongozi wa vyama husika tuweke mifumo mipya itakayoweza kubuni mbinu za kuleta maendeleo kisoka na michezo mingine bila hivyo ,Tanzania itapitwa hata na sudan kusini ambao ndio taifa jipya katika soka afrika.    
    


No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers