HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

22 May 2013

TANZANIA YANG'ARA KUOGELEA KENYA

Timu ya vijana ya kuogelea kutoka Tanzania imefanya vizuri katika mashindano yaliyoshirikisha timu 20 kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki na mashindano hayo kufanyika jijini Nairobi kuanzia tarehe 17 hadi 19 May 2013 katika shule ya Aga Khan. Washiriki wa mashindano hayo walitoka katika nchi za Tanzania, Kenya, na Uganda ambazo kila mmoja alitaka kumshinda mwenzake. 

Wasichana kutoka Tanzania wamekuwa washindi wa kwanza kwa kupata alama176 points dhidi ya timu 24. Timu ya Uganda Dolphins imeshika nafasi ya pili  kwa kupata alama 148 ambao walijaribu kuonyesha upinzani kwa timu yetu. Timu ya Tanzania kwa upande wa wanaume imeshika nafasi ya 6 dhidi ya timu za wanaume 19 zilizoshiriki katika mashindano hayo. Hii ilisababishwa na ukweli hatukwenda na wachezaji wa kutosha kiasi hawakuweza kushiriki katika relay na tulipata alama 54. Matokeo ya jumla ni kuwa Tanzania tumekuwa watatu kwa kupata alama 230 ambapo Dolphins Uganda wamekuwa wa kwanza kwa kupata alama 278 na Makini ya Kenya wapili kwa kupata alama 240.50.
Waogeleaji wetu walikuwa na ari ya juu licha ya hofu tulikuwa nayo hapo kabla ya baridi kali na tunamshukuru Mwenyezi Mungu hakukuwa na baridi kali labda wakati wa usiku. 

Muda wote wa mashindano waogeleaji wetu wakati wanapiga mbizi walishangiliwa kwa sauti ya juu na shukrani kwa wazazi ambao muda wote walikuwa wanashangilia ``Tanzania oye``. Kwa hakika ni matokeo ya kufurahisha licha ya medali,  wachezaji wetu waliweza  kushusha muda wao na kuweka muda mpya(PB)na wengine wameteremsha muda wao hadi sekunde 10. Waogeleaji wetu walikuwa walikuwa katika kiwango bora kuanzia siku ya mwanzo ya mashindano walipoanza kuogelea mita 100 (IM) muogeleaji anaogelea stroke zote 4. (25m butterfly, 25m backstroke, 25m breastroke and 25m freestyle).
Kila aliyeshiriki alikuwa anajaribu kumshinda mpinzani wake na kwa kweli tulikuwa na ushindani mkali kutoka kwa waganda na wakenya . Muogeleaji  Sonia Tumiotto (KAPTENI WA TIMU) alipata dhahabu na kuweka rekodi ya mashindano kwa wasichana miaka 11 mita 100 IM kwa kuogelea muda mpya wa dakika 1:18:70. Medali ya silver ilienda kwa  Smriti Gokarn ambaye alikuwa na upinzani mkali kutoka kwa wasichana wenzake miaka 10 na kuogelea muda wa dakika 1.25.54
Siku ya pili ya mashindano hayo waogeaji wetu waliweza kupata mbalimbali wakiwemo. Selina Itatiro (silver, miaka 9 wasichana, 25m fly), Tessa Francis (bronze, miaka 9 wasichana 25m fly, na silver 25m free), Smriti Gokarn (silver, 50m fly. Silver 50m breast, dhahabu 50m back, silver 25 free), Sonia Tumiotto(11) (Dhahabu, 50m fly, dhahabu 50m breast, dhahabu 50 back, dhahabu 25 free), Amani Doggart (bronze miaka 8 wasichana 25m breast) ,Njukia kihara (silver, miaka 7 breast), Dhashraad Magevaran (10)(bronze, 50m back).
Waogeleaji wetu pia wamekuwa washindi na kupewa zawadi ya vikombe kwa kila umri. Waliopata vikombe kwa wasichana miaka 8 ni Amani Doggart nafasi ya tatu, Tessa Francis miaka 9 wasichana nafasi ya tatu, Smriti Gokarn miaka 10 nafasi ya pili na kuweka rekodi mbili na Sonia Tumiotto miaka 11 wasichana nafasi ya kwanza na kuweka rekodi 3.
Siku ya jumapili ilikuwa ndio siku muhimu na ya kweli kwa Tanzania ambapo waogeleaji wa relay waliweza kupata dhahabu kila tukio tuliloshiriki. Katika miaka 8 wasichana kwa timu ya relay iliyowashirikisha   Diya Patel, Maia Tumiotto, Ursula Khimji and Amani Doggart walipata dhahabu mbili kwa medley relay(KILA MUOGELEAJI ANAOGELEA AINA MOJA YA MTINDO WA KUOGELEA) na freestyle relays, wasishana wa miaka 11 yenye waogeleaji Sonia Tumioto, Selina Mehta, Maya Kihara, Tallin Stengell nao waliweza kuchukua medali mbili za dhahabu kwa medley relay na  freestyle relays. Miaka  10 wavulana kwa tim u yenye waogeleaji  Dhashraad Magesvaran, Urav Shah, Alexander Belikov and Vansh Ladwa nao walichukua dhahabu katika mtindo wa medley relay  and freestlye relays. Juhudi za pamoja kati ya wasichana na wavulana ndizo zilizotuwezesha Tanzania kuwa nafasi ya tatu kwa  matokeo ya jumla kwa mwaka 2013
Naye kocha wa timu hiyo Mohamed Abdulazizi alisema kuwa “Tuliwaandaa wachezaji kimwili na kiakili kuweza kukabiliana na lolote litakalojitokeza mbele yetu ndio siri ya mafanikio haya ya kufurahisha.
Tanzania iliwakilishwa na Sonia Tumiotto (Team captain), Harry McIntosh (vice captain), Dashraad Magesvaran (boys captain), Smriti Gokarn (girls captain), Reuben Monyo, Njukia Kihara, Prashraad Magesvaran, Oliver McIntosh, Shiv Shreekumar, Gian Maria, Vansh Ladwa, Alexander Belikov, Urav Shah, Maia Tumiotto, Diya Patel, Amani Doggart, Celina Itatiro, Tessa Francis, Janice Njuguna, Selina Mehta, Maya Kihara, Mariana Pipollo, Piya Shah, Talin Stengel and Ursula Khimji. Makocha wengine wqa timu hiyo ya waogeleaji 25 walikuwa ni Kocha Alex Mwaipasi na Kocha Kanis Mabena na Mkuu wa msafara alikuwa ni Inviolata Rwelamira Itatiro. 

Tunajivunia vijana hawa kwa kutuwakilisha vyema na kufanya Tanzania kungára, Hongera sana  pamoja na wazazi wote. Hii ni mara ya pili katika historia ya mchezo wa kuogelea ambapo timu ya vijana imeweza kwenda kushiriki mashindano ya Afrika Mashariki na kurudi na vikombe na medali nyingi. Mara ya kwanza ilikuwa timu ya vijana pia ilipoweza kurudi kwa kikombe cha mshindi wa pili baada ya kujikusanyia medali 76 ambapo mashindano hayo yalifanyika Kampala mwezi wa 10 tarehe 22 na 23 mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers