Kamati
ya kusimamia Tuzo za Wanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2012
zinazotolewa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania
(TASWA) imepokea mapendekezo ya majina ya wanamichezo kutoka vyama
mbalimbali kwa ajili ya kuwania tuzo hizo kwa kila mchezo.
Majina
ya wanamichezo hao yamependekezwa na vyama husika, isipokuwa mpira wa
miguu kwa wanaume pamoja na mpira wa kikapu, ambapo majina yameteuliwa
na kamati kwa kushirikiana na baadhi ya wahariri wa habari za michezo na
wadau wa michezo husika, ingawa awali vyama hivyo viliombwa kuwasilisha
majina lakini havikutekeleza ombi hilo hivyo kamati ikaamua kutafuta
utaratibu mwingine wa kupata majina.
Pia
vyama viwili vya michezo ya paralimpiki na baiskeli bado majina
hayajaifikia kamati yetu kutokana na sababu mbalimbali na tayari
wameahidi watawasilisha majina hayo kabla ya Mei 12 mwaka huu. Chama cha
Mpira wa Wavu pia kimeshindwa kuwasilisha majina.
Hatua
ya mwisho ambayo itafanyika baada ya kupokea mapendekezo hayo kwenye
kila mchezo, Kamati ya Tuzo za Taswa itafanya uchambuzi kupitisha majina
hayo kulingana na sifa ambazo vyama husika vimeleta kwa kila
mwanamichezo na kuona kama wanastahili kupewa tuzo kulingana na vigezo
vya kamati na TASWA.
Awali
TASWA ilipanga tuzo hizo zifanyike Aprili 27 mwaka huu, lakini
imeshindikana kutokana na sababu mbalimbali zilizokuwa nje ya uwezo wa
Kamati ya Tuzo pamoja na chama kwa ujumla na sasa sherehe zitafanyika
mwanzoni mwa mwezi Juni katika tarehe itakayotangazwa baada ya
kukubaliana na wadhamini, ambapo mazungumzo yanatarajiwa kukamilika
kabla ya Mei 15 mwaka huu.
Tunavishukuru
vyama vyote vilivyotupa ushirikiano kwa hatua ya awali kwa kutupatia
mapendekezo yao pamoja na kutaja sifa kwa kila mchezaji waliyewasilisha
jina lake nasi tunaahidi tutapitia kwa umakini mapendekezo hayo, lakini
uamuzi wa kamati ndiyo utakaokuwa wa mwisho.
TASWA
itatoa tuzo kwa kila mchezo ambao kamati yetu ambayo Katibu wake ndiye
pia Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando itajiridhisha wanastahili, ambapo
baadaye washindi wa kila mchezo watawania Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa
Tanzania kwa Mwaka 2012.Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Tanzania kwa mwaka
2011 ilienda kwa Shomari Kapombe. Washindi wengine kwa miaka ya karibuni
ni Mwanaidi Hassan (2010 na 2009), Mary Naali (2008), Martin Sulle
(2007) na Samson Ramadhan (2006).
Majina ya wanaowania kwa mwaka 2012:
MPIRA WA MAGONGO-WANAUME
1 Sylvester Kigodi
2. Casto Mayuma
3. Gurtej Bilu Singh
4. Vendri Bhamra
5. Elias Samala
GOFU YA KULIPWA
1 Hassani Kadio
2 Yassin Salehe
3 Fadhili Nkya
4 Salimu Mwanyenza
5 Rajabu Iddy
GOFU YA RIDHAA WANAWAKE:
1:MADINA IDDI
2:ANGEL EATON
3. HAWA WANYECHE
4.AYNE MAGOMBE
GOFU YA RIDHAA WANAUME
Jimmy Mollel
Frank Roman
Nuru Mollel
Martin MacDonald
John Said
NGUMI ZA RIDHAA-WANAUME
Ismail Isack Galiatano
Said Hofu
Selemani Kidunda.
Victor Njaiti
Mohamed Chibumbui.
NGUMI ZA RIDHAA WANAWAKE:-
1. Sara Andrew
2. Irene Kimaro
3. Easter Kimbe.
4. Mather George
5. Mariam Nyerere.
NGUMI ZA KULIPWA
1. Francis Miyeyusho
2. Ramadhan Shauri
3. Thomas Mashali
4. Said Mbelwa
5. Francis Cheka
JUDO-TANZANIA BARA-WANAUME
1) AHMED MAGOGO
2) ADREW THOMAS MLUGU
3) GEOPHREY EDWARD MTAWA
4) GERVAS LEONARD CHILIPWELI
5) ABUU SELEMANI MCHETEKO
6) ABUUBAKAR NZIGE
JUDO TANZANIA BARA WANAWAKE
1. MATRIDA .H. TEMBA
2. AMINA MOHAMED
JUDO ZANZIBAR-WANAUME
1. MOHAMMED KHAMIS JUMA
2. MASOUD AMOUR KOMBO
3. MBAROUK SULEIMANI SULEIMAN
JUDO ZANZIBAR-WANAWAKE
1. GRACE ALPHONCE
2. LAYLATI MOHAMMED
TENISI-WANAWAKE
[1] Rehema Athumani
[2] Vailety Petar
[3] Mkunde iddi
[4] Edna John
[5] Zuhura Baraka
TENISI WANAUME
[1] Omary Abdalah
[2] Yassini Shabani
[3] Hassan Kasimu
[4] Kiango Kipingu
[5] Lebric Jacobu
MPIRA WA MIKONO-WANAUME
Faraji Shaibu
Nyuki ZANZIBAR
Hemedi Salehe
JKT
Abinery Kusena
JKT
Ally Khamis
Ngome
Hassani Yusufu
Magereza
MPIRA WA MIKONO-WANAWAKE
Catherine Mapua
Ngome
Dorisi Mangara
Magereza
Zakia Mohamed
Ngome
Happy Mahinya
JKT
Mary Kimiti
Magereza
RIADHA-WANAWAKE
1.Zakia Mrisho
2. Mary Naali
3.Jacklin Sakilu
4.Sarah Ramadhani
5.Anjelin Tsere
6. Sara Maja
RIADHA-WANAUME
1. Dickson Marwa
2. Faustine Musa
3. Augstino Sule
4. Bazil John
5. Samson Ramadhan
KRIKETI-WANAUME
1. Abhik Patwa.
2. Benson Mwita.
3. Sefu Khalifa.
4. Issa Kikasi.
5. Riziki Kiseto
KRIKETI-WANAWAKE
Monica Pascal.
Mwanaiddi Ibrahim.
Hadija Nasibu
Esther Wales
Mwanaidi Ammy
SOKA-WANAWAKE
FATUMA MUSTAPHA
ASHA RASHID
MWANAHAMISI OMARY
SOPHIA MWASIKILI
ESTER CHABRUMA
SOKA-WANAUME
JOHN BOCCO-AZAM
KELVIN YONDANI-YANGA
SHOMARI KAPOMBE-SIMBA
MCHA KHAMISI-AZAM
MBWANA SAMATTA-TP MAZEMBE
Thomas Ulimwengu-TP Mazembe
WACHEZAJI WA NJE WANAOCHEZA TANZANIA
EMMANUEL OKWI-SIMBA(SASA ETOILE DU SAHEL)-SOKA
KIPRE TCHETCHE-AZAM-SOKA
HARUNA NIYONZIMA-YANGA-SOKA
HAMISI KIIZA-YANGA-SOKA
MARY WAYA-FILBERT BAYI –NETIBOLI (ALIKUWA KOCHA MCHEZAJI)
KIKAPU-WANAWAKE
Faraja Malaki- Jeshi
Evodia Kazinja-JKT Stars
Sajida Ahmed-Don Bosco
Rehema Kilomba-Donbosco
Tukusubira David-Vijana Queens
KIKAPU-WANAUME
Mussa Chacha-Savio
Lusajo Samuel Mwakipunda-Oilers
Salim Mchemba-ABC
Filbert Mwaipungu-ABC
Steven Atanasio-ABC
NETIBOLI
Lilian Sylidion-Filbert Bayi
Mwanaidi Hassan-JKT
Irene Elias Kanile-Filbert Bayi
Jacqueline Sikozi-Filbert Bayi
Faraja Malaki-Jeshi Stars
WACHEZAJI BORA CHIPUKIZI
Salum Abubakari-Azam-soka
Frank Domayo-Yanga-soka
Edward Cristopher-Simba-soka
Emmanuel Malya-Tenisi Gymkhana Arusha
Tambwe Juma-Kriketi
WATANZANIA WANAOCHEZA NJE
Mbwana Samatta-TP Mazembe
Ivo Mapunda-Gor Mahia
Hasheem Thabeet-Oklahoma
Thomas Ulimwengu-TP Mazembe
Soud Abdulrazak-Uganda (kikapu)
Mohammed Abdallah ‘dulah’-Uganda (kikapu)
TUZO YA HESHIMA— ITATANGAZWA UKUMBINI
TUZO YA MWANAMICHEZO BORA MWAKA 2012- ATAPATIKANA MIONGONI MWA WASHINDI WA KILA MCHEZO.
No comments:
Post a Comment