HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

29 August 2013

Dkt. Fenella Mukangara TAZAMA UZURI HAWAKAWII KURUSHA KONDE !!!


FENELLA-1
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akielezea kufurahiswa kwake na ukuaji wa mchezo wa ngumi hapa nchini alipokutana na  Bondia maarufu duniani na aliyewahi kuwa bingwa wa dunia mara mbili Francois Botha (White Buffalo) jijini Dar es Salaam.
FENELLA-6
Bingwa wa dunia mara mbili wa mchezo wa ngumi Bondia Francois Botha (White Buffalo) akielezea jambo kwa waandishi wa habari alipotembelea ofisini kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara (kulia) jijini Dar es Salaam.
FENELLA-2
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiwa na  Bingwa wa dunia mara mbili wa mchezo wa ngumi Bondia Francois Botha (White Buffalo) akikabidhiwa zawadi ya picha ya bondia huyo ikionyesha enzi za ujana wake. 
FENELLA-4
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Wizara na wageni walioambatana na bondia Botha .(Picha na Frank Shija – Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo).

FENELLA-&

 Bingwa wa dunia mara mbili wa mchezo wa ngumi Bondia Francois Botha (White Buffalo) akielezea jambo huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Sihaba Nkinga akisikiliza kwa makini. Botha yupo nchini kufuatia kuwepo kwa pambano la ngumi la dunia litakalofanyika kesho likiwakutanisha mabondia Francis Cheka wa Tanzania na Phill William wa Marekani.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers