Mlinda Mlango wa Timua ya soka ya Taifa ya Nigeria , Vincent Enyeama, amekanusha Tetesi zilizoenea kuwa ameachana na soka ya Kimataifa katika hafla ya Tuzo za mwaka za Ibom katika jiji la Uyo.
Enyeama amesma Hajatangaza kabisa kustaafu soka ya kimataifa na jambo hilo ni la kushauliana yeye na familia yake .
“Sijasema kuwa sitachezea tena Nigeria maarufu kama Tai wa Kijani.Nilichosema ni kwamba nitakaa chini kushauriana na familia yangu na hilo jambo la kawaida . Mimi bado ni mchezaji wa timu ya taifa ,”amesema Mlinda mlango huyo wa Lille .
“Nimefurahishwa sana na Zawadi hii .na ninawashukuru sana waandaji wa Tuzo hiii. Nimeshinda tuzo nyingi sana lakini kupewa tuzo na watu wa nyumbani kwetu kijiji nilichozaliwa Akwa Ibom ni jambo la kujivunia sana .
“Mambo mazuri huanzia Nyumbani Hili ni jambo kubwa sana kwangu na lina maana kubwa kwangu .Nifanya kazi kujituma zaidi ili nifanikiwe zaidi ,” Anasema Enyeama .
,Mlinda Mlango Huyo alicheza vizuri sana katika michuano ya Kombe la Dunia 2014 Tangia hapo Vilabu kadhaa Vimekuwa Vikihitaji huduma yake moja ya Klabu hizo ni
Manchester United, West Ham United, Arsenal na Tottenham.
No comments:
Post a Comment