Kikosi cha Taifa Stars kinatarajia
kuondoka keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Mbeya ambapo kitapiga kambi ya
wiki moja kujiandaa kwa mechi ya marudiano dhidi ya Msumbiji.
Mechi hiyo ya raundi ya pili ya
michuano ya Afrika kutafuta tiketi ya kushiriki Fainali za Afrika (AFCON)
zitakazochezwa mwakani nchini Morocco itafanyika wikiendi ya Agosti 2 na 3
mwaka huu nchini Msumbiji.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro
Premium Lager itaondoka nchini Julai 31 mwaka huu kwenda Johannesburg, Afrika
Kusini ambapo itafanya mazoezi ya mwisho kabla ya kutua Maputo kwa ajili ya
mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa wa Zimpeto.
No comments:
Post a Comment