Baadhi ya wanasiasa wakubwa Nchini Ujerumani akiwemo Kiongozi wa Nchi hiyo Angela Merkel’ ambaye anaongoza chama kisichopenda mabadiliko ameongeza joto la kutaka kupokwa kwa Urusi kunyang'anywa kuandaa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika mwaka 2018 baada ya kutunguliwa kwa Ndege ya Malaysia iliyokuwa ikipita katika Anga la Ukrane.
Nchi za Magharibi wamekilaum kikundi kinachosadika kuwa kinatoka urusi katika kupinga jimbo la Kiev’s kujitoa mashariki mwa Ukraine Baada ya Kuitungua Ndege ya Malaysia Airlines MH17 siku ya Tarehe 17 July Ambapo jumla ya watu 298 waliuawa.
Umoja wa ulaya bado unataka kuweka Vikwazo zaidi vya kiuchumi kwa Nchi ya Hiyo ambapo jana Jumanne mawaziri walichelea kufanya maamuzi na watasubiri kwa siku kadhaa .
Kuipokonya Urusi kuandaa kombe la Dunia itakuwa suluhisho zuri zaidi la kiuchumi kuliko kuiwekea Vikwazo cha Kiuchumi , Alisema Michael
Fuchs, Ambaye ni makamu kiongozi wa chama kisipenda mabaliko Katika Bunge la Ujerumani .
“Fifa
Inatakiwa kufikiria kuhusu Moscow kama kweli inaweza kuandaa mashindano kwani imeshindwa hata kutoa uhakika wa Anga yake katika usafiri wa Ndege ,” Fuchs ameliamba gazeti moja la Handelsblatt Online, Amesema Ujerumani na Ufaransa wanaweza kuandaa michuano hii kwa haraka sana .
Vikwazo vya Kiuchumi hawezi kuikaba sana Urusi ukizingatia Urusi ina mipaka mikubwa sana ,
Ambayo ni migumu sana kulinda Bidhaa mbalimbali zisiweze kuingizwa nchini humo , .
Vyama vya biashara vya Ujrerumani vimesema kuwa Vikwazo vya Umoja wa Ulaya EU vinaweza kuharibu uchumi kati ya Russia na Ujerumani ,Kwani Ndio Nchi ambazo zinakamata Uchumi mkubwa wa Ulaya .
Waziri wa mambo ya Ndani katika jimbo la Hesse amekubarina na kauli ya Fuchs.
“Kama
[Rais wa Urusi Vladimir] Putin aonyeshi ushiriakiano kabisa katika jambo kubwa la kutunguliwa kwa Ndege , Michuano ya kombe la Dunia kufanyika Urusi 2018 ni ya kufikirika ,” Peter Beuth amelimbia Gazet hilo la Ujerumani la Bild.
Stephan
Mayer, Ambaye ni mwanachama wa Chama cha kijamii cha umoja wakristo wasiotaka mabadiliko(CSU),Amesema kuindoa Urusi kutoandaa michuano ya Kombe la Dunia ni jambo safi kabisa.
Chama soka cha Ujerumani (DFB) hakikuwa Tayari kutoa maoni katika mjadala huo ulioitishwa Bungeni siku ya jumamatano kwa maoni yaliyotolewa na wanasiasa ’ .Ujerumani ndio mabingwa wa Dunia wa michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika Nchini Mwaka huu Brazil.
Ndege hiyo ya Malaysian ilikuwa ikitoka
Amsterdam Kuelekea Kuala Lumpur na baadae ikatunguliwa maeneo ya Donetsk, ambapo ni ngome ya kuu ya vikosi vya Urusi Dhidi ya Ukraine .
Ambapo Abiria wengi waliokuwemo kwenye Ndege hiyo walikuwa wakitokea Uholanzi , Chama cha soka cha uholanzi kimesema kuwa ni mapema sana kujadiri uhalari wa Urusi kuandaa michuano hiyo 2018 .
“Chama soka cha Uholanzi kimesema kuwa kinaelewa kuwa watu wa uholanzi wanaelewa kumbukumbu mbaya ambayo imetokea katika maisha yao ,” .
“Chama hicho kinaamini kuwa sio jambo sahihi kwa sasa kuzungumiza michuano mpaka uchunguzi utakapo kamilika , ”
Chama soka cha Uingereza kimesema Ni mapema sana kuzungumzia uwezekano wa kuondoa michuano hiyo huko Urusi.
No comments:
Post a Comment