HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

21 July 2014

NAHODHA WA TIMU TAIFA YA UINGEREZA Steven Gerrard: ASTAAFU SOKA YA KIMATAIFA

Nahodha wa Timu ya Taifa ya Uingereza  Steven Gerrard amestaafu kucheza soka ya Kimataifa baada ya kuitumia Uingereza mara 114.
Gerrard, 34, alicheza mechi yake ya kwanza mwaka 2000 na Kupata Ushindi wa  2-0 Dhidi ya Ukrane  Aliichezea Uingereza kwa mara ya Mara Mwisho mwaka 2014 kwenye Kombe la Dunia  na kupata Suluhu ya  0-0 Dhidi ya  Costa Rica.
"Nimefurahia kila dakika ya Kuiwakilisha Nchi Yangu .Ni siku ya Huzuni kwangu  ," Kiungo huyo wa Wa  Liverpool amesema ".
Gerrard sasa atakuwa anabeba majukumu ya kuwa Balozi wa chama cha soka cha Uingereza kimataifa . 

Kiungo huyo wa kimataifa wa Uingereza ameifungia Timu yake mabao  21wakati alipoiwakilisha timu yake ya taifa katika mashindano sita tofauti .  
"Ulikuwa Uamuzi mgumu sana kuufanya. Ni jambo ambalo nilikuwa nikilitafakari kwa Muda Kidogo, sio mara baada ya  kombe la Dunia kumalizika   ,"Kiungo huyo wa  Liverpool amesema .
"Nilitaka shauri mbalimbali kutoka kwa watu wangu wa karibu  -Wachezaji ambao ninacheza nao , Wachezaji wa zamani ambao nilicheza nao zamani , Makocha ambao nilikuwa nao miaka kadhaa iliyopita . 
"Huu umekuwa uamuzi mgumu sana, Ni moja kati ya maamzuzi magumu ambayo nimewahi kuyafanya Tangu nilipotimu miaka 18 na kuwa Mchezaji wa kulipwa ."
Gerrard ataendelea kuitumiakia klabu yake  Liverpool, ambayo ndiyo alinaza nayo kuchezea mwaka 1998 Dhidi ya   Blackburn Rovers.
Mwandishi mwandamizi wa BBC michezo  Phil McNulty anasema : "Gerrard alivunjwa moyo Baada  kutolewa kwa uingereza katika mechi  michuano ya kombe la Dunia na sasa hatokuwemo katika michuano ya ulaya ya mwaka   2016 itakayofanyika Ufaransa . 

"Kwa uwezo mkubwa alionao ,Amesikitishwa na matokeo waliyoyapata Nchini   Brazil na ilikuwa wazi kuwa kijana 34-na aliona kuwa uwezo wake ulikuwa unampa mkono wa kwaheri ."

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers