James Rodriguez amewasili Katika uwanja wa Ndege wa Barajas huko Madrid akiwa anajiandaa kujianga na Real Madrid ya Uispania .
Mkolombia huyo -Alikuwa akiichezea klabu ya Monaco - akiwa anatokea kwenye Michuano ya Kombe la Dunia baada ya kung'aa na timu ya taifa ya Colombia akifunga Mabao sita.
Tangu hapo amekuwa akihushswa na kuhamia Klabu maarufu Dunia na wanaotumia pesa Nyingi Duniani yenye maskani yake katika uwanja wa Bernabeu, Huku Manchester United Ikiwa nayo imevutiwa na Huduma ya Mchezo huyo .
Mabingwa hao wa Ulaya walipata hoja ya Nguvu kwani juma lililopita Gazeti moja la UiSpania lilikaririwa likisema kuwa Real na Monaco wamekubaliana na kulipana Dau la £63million.
Na sasa inaoneka kuwa kuna uwezekano mkubwa wa Kiungo huyo kuhamia Madrid na ameonekana katika uwanja wa Ndege wa Barajas huko Madrid.
Mapema alionekana kuondoka katika jiji la Medellin akielekea Uispania na mjadala ukionekana Kufungwa .
MColombian alijiunga na Monaco kwa £38million mwaka jana na ameonekana kupanda Bei mara baada kufanya Vizuri katika Michuano ya Kombe la Dunia.
No comments:
Post a Comment