Mwaka 2014 Ujerumani imetwaa Ubingwa
wa Dunia katika Ardhi ya America ya
Kusini ni kwa miaka zaidi ya Sabini na Minne wameweza kuvunja Rekodi hiyo na
kwa wasiyojua Historia Mjerumani Ndiye aliyetawala zaidi Tanganyika ambayo sasa inaitwa Tanzania
lakini kabla ya majina yote hayo Tanzania ilikuwa ikiitwaa Deutsostafrika yaani Dola ya Kijerumani
afrika mashariki wanaojua Historia watakuwa wanajaribu kunielewa.
Nchi ambayo nimekutajia ilipata kuwa
na kiongozi mmoja makini na Mjanja sana Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
ambaye mimi kila napomkumbuka Mzee huyu nakumbuka majina kama Mwitongo,Burito
kwa wenyeji wa Mkoa wa mara mtakuwa mnajua maana ya Majina hayo na maana yake , Mzee
huyu aliwahi kunukuliwa akisema hivi “Itachukua Miaka mia moja na Themanini
Mtanzania wa kawaida kuwa sawa na Mjerumani “.
Watu walilitazama jambo kama mzaha na
wengine wakisema Mzee Yule ni muongo lakini mimi nina ungana nae na kuongeza
kuwa Imebaki miaka mia moja thelathini Tanzania itwae Ubingwa wa Dunia hii
ukianzia Tangu tulipopata uhuru December 9/61 mpka leo sababu tumeshekherea
miaka hamsini ya Uhuru na Bado hatuja waweza kucheza robo fainali ya Mataifa ya
afrika ,Na Mfano mzuri ni kuwa mara ya kwanza Tanzania ilikuwa inacheza Bila jezi hiyo ilikuwa miaka ya Nyuma .
Kuna mambo mengi ambayo Tanzania
hayaja kaa sawa mpaka Muda huu kama Elimu,Afya,Miundo Mbinu ,Na la mwisho
ambalo ndilo hatuna kabisa ustaarabu mambo haya Mjerumani anayo Kabla kombe la
Dunia Halijaaanzishwa sisi Mambo hayo mpaka leo Bado hatuna au Tunafanya
Kinyume.
Kwa Mfano Elimu Anayepata Divisheni 4
anakuwa mwalimu anaenda kuwafundisha kufeli wanafunzi wengine kwa hiyo tunazidi
kuongeza wajinga kila sehemu tunakuwa na wanamichezo wajinga wasioelewa namna
ya kujilinda kimichezo wasiofundishika na
ukiwaletea kocha mzungu ndio kabisa maana wa Kiswahili tu hawamwelewi!
Na Walio wengi ambao wamepata Idea ya kusoma na wakaelewa wengi wao wapo Dar Es
salaam .
Lakini huko mikoani kwenye Vipaji Vingi zaidi kuna mamia ya mambumbu wasio jua
lolote kwa sababu hata mwalimu ukimpangia shule mkoani haendi kisa hajaingiziwa
Pesa na miundo Mbinu mibovu je mpaka mambo haya yakae sawa ujerumani itakuwa
ishatwaa Ubingwa mara Ishirini na Tano Brazil Arobaini Tanzania inaweza kuwa
imshafuzu labda mara nane kucheza kombe la Dunia tena Bila kushinda mechi
yoyote kwenye makundi lakini kwa hari ilivyo inaonekana kadri ujerumani
inavyozidi kuendelea Ndivyo Tanzania inavyozidi kuwa maskini Je unadhani
kuna maendeleo ya soka kweli ?
Mpaka sasa kuna wachezaji kama Haruna
Moshi, Shomari Kapombe , Mrisho Ngasa ambao wameshawahi kwenda ulaya kujaribu kucheza
soka na wamechemka lakini kuna wakenya ambao wanaongezeka Tanzania na wanazidi
kwenda ulaya na wanazidi kutwaa medali kadhaa katika mashindano ya kimataifa
hii ina maana mwalimu Nyerere alishajionea haya miaka iliyopita je tangu
amefariki kipi tumefanikiwa mpaka sasa kama wajinga wanazidi kuongezeka miundo
mbinu haija kaa sawa Je nasema Uongo kuwa Nyerere Hakukosea !
Hivi
Ni kipi ambacho hasa tunajvunia katika michezo ukitazama Zimebaki Story
aah Mwaka Themanini Tulifuzu mataifa ya Afrika Nigeria ,Aaah Nyambui
Alileta Medali Madola na Filbert Bayi alileta Medali Na hata ilifika
fainali kombe la Shirkisho baada ya hapo Rais Mstaafu Alhaji Ally Hassan
Mwinyi akasema Tanzania Itaendelea kuwa Kichwa cha Mwendawazimu
anaejiskia Kunyoa Basi ananyoa na Ndio Kauli Pekee ambayo Tanzania
Tunaweweseka nayo kwani Mzee mwinyi aliitoa kwa Uchungu sana na ilitoka
Moyoni kisa tulifungwa Mbele yake kwa sababu tu kuna Baadhi ya wachezaji
inasemekana walifungisha Je? wachezaji hao walikuwa na Elimu ya Kutosha
jibu hawakuwa nayo wangekuwa nayo wasingekubari.
Kwa hiyo bado miaka Mia Moja na Thelathini kwa Tanzania Kuchukua Kombe la Dunia ..
No comments:
Post a Comment