HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

4 August 2014

Maximo, Poulsen, Kpoulsen, Ignatius na wachezaji ni wale wale nini Tatizo????







 


Image result for Marcio Maximo
Timu ya taifa inaangaika utafikiri mgonjwa ambaye anaumwa maradhi yasiponyeka na Muda wowote anasubiriwa Israel Mtoa Roho tu Aje aitimishe safari ili iingie kaburini yanaweza kuwa maneno makali sana kwenye macho yako kuyasoma lakini hii ndivyo hari ilivyo kwani sasa unaweza kujionea wazi labda niulize swari ni kocha au wachezaji Ndio wenye matatizo  kwani ni mchezaji gani ambaye hakuwemo Tangu wakati wa Maximo ukianzia Golini mpaka wafungaji?

Kwanini Mariga ,Wanyama,Oriech ,Origi wanacheza soka ulaya kwanini Kapombe kashindwa ufaransa? Kwanini Haruna Moshi kashindwa Sweden? ,Kwanini Ngasa kashindwa Uingereza? Kwanini nizar Khalfan Karudi Kutoka Canada? kwanini tunakimbilia Arabuni kila siku Kuna tatizo Gani ?
Mimi leo nakueleza Ukweli wachezaji wa Tanzania Uwezo wao ni mdogo Tangu maximo alipochukua Timu aliita wachezaji wangapi Timu ya Taifa Ukihesabu sasa wanaweza kufika hata Hamsini lakini Bila bila Mchezaji wa Mpira wa Miguu anatunza kiwango cha soka kwa kiwango chake mwenyewe na sio timu mwaka 2002 Uingereza ilikuwa kundi Moja na Sweden wachezaji wa Sweden walikuwa wakicheza katika ligi Daraja la pili uingereza unadhani kwanini waliweza kuisimamisha uingereza ni kutokana na uwezo sina maana ya kufananisha hapana najalibu kukupa mfano tu.

Wachezaji wengi watanzania  Wamefeli shule !wengi Darasa la saba na kidato cha Nne  je watamuelewa kocha kama kuna mchezaji ambaye ana Digrii anyooshe Mkono sidhani kama kuna mtu atanyoosha mkono kiukweli wachezaji watanzania ni wabishi kuelekea wao wenyewe ni makocha kuwakacha walimu lakini Jamani Hivi Tanzania hakuna kocha ? asilimia kubwa ya Timu za zote Zinafundshwa na wazawa ukiacha timu Kubwa Mbeya city ambaye alikuwa akitishia usalama wa watu inafundishwa na Mzawa Juma Mwambusi Lazima tutazame ni kweli Maximo hajui kufundisha,Jan na Kim hawajui kufundisha Mart naye hajui kufundisha ?
Ukiacha Darasa moja linabadilishwa walimu kila siku wanafunzi wale wale juaeni kuwa mnampigia Mbuzi gitaa .
Malinzi pole sana naona una kazi kuliko kocha ukitazama huku makocha inaonekana huna waamuzi huna wachezaji short kozi Sijui kama timu unayo? Miundo mbinu je ?
Labda tuulize swali dogo tunataka kitu gani kwasababu mipango Midogo tumeshindwa kwa mara nyingine tena mipango ya Muda Mfupi imechemka kwenda Afcon ,Inashindwa kutwaa chalenji,inashindwa kwenda kombe la Dunia je tunataka mpango wa Muda mfupi kwa ajiri ya kitu gani ni nchi gani imefanikiwa kutwaa au kushiriki michuano mikubwa kwa mipango mifupi ?kwanini tusijaribu wa Muda Mrefu ?
Hivi ni kweli timu ya Kenya inatuzidi kiwango au ni uzembe wa wachezaji wetu tu

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers