HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

3 September 2012

Mahmoud el Gohary Atangulia mbele ya haki 74

Mahmoud el-GoharyKocha wa mpira  wa miguu

  Mahmoud el Gohary amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 74 baada ya kuugua ugonjwa wa kiharusi huko Jordan shirika la habari la MENA limethibitisha
El Gohary ambaye ni moja kati ya alama kubwa ya soka la misri alikuwa kocha mkuu wa timu hiyo  pale ma Pharaoh walipocheza fainali zao za mwisho za kombe la dunia mwaka 1990 ambapo aliiiongoza timu hiyo kutoa suluhu ya goli moja kwa moja dhidi ya mabingwa wa ulaya mwaka 1988 uholanzi huko italia huku akipta umaarufu kwa kuwa na ngome ngumu kiwanjani
, El Gohary ndie aliyeipatia Misri kombe la mataifa ya Afrika mwaka 1998 kule ougodougo Bukinafaso  .
El Gohary  aliwahi kufundisha timu za taifa za Oman ,Jordan na Misri ,na aliwahi kuifikisha Jordan hatua ya robo fanali katika kombe la asia mwaka 2004 na aliwahi kuwa mshauri katika shirikisho la soka la Jordan mwaka 2009
katika ngazi ya klabu ameshinda vikombe vya nyumbani na vya kimataifa akiwa na timu za mji mmoja wa Cairo
  Al Ahly na Zamalek,ikiwa pamoja ligi ya misri na ligi ya mabingwa barani afrika vile vile aliwahi kuchezea vilabu vikubwa vya nchi hiyo
  Al Ahly katika miaka  1955 na  1961, lakini majeruhi yalimsabisha astaafu soka
El-Gouhari  ameacha mke na watoto wa tatu .

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers