HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

1 September 2012

WAAMUZI TANZANIA WAPATA SOMO


Mkurugenzi wa ufundi wa Shirikisho la soka la Tanzania TFF Sunday Kayuni akitoa wosia kwa  waamuzi kabla ya kuanza majukumu yao katika  ligi kuu Tanzania Bara

MKURUGENZI wa Ufundi wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Sunday Kayuni amewaasa waamuzi kutumia filimbi yao vizuri ili kutenda haki wanapo kuwa uwanjani.

Kayuni aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa  semina ya waamuzi wa daraja la kwanza kituo Dar es salaam inayofanyika Uwanja wa Taifa, kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara, msimu wa 2012/13.

Amesema waamuzi ni kiungo muhimu  katika kuendeleza mpira nchini, endapo watakuwa mahakimu wazuri wakiwa uwanjani.

Amewataka waamuzi hao  kuchezesha kwa kufuata sheria 17 za soka, ili waweze kusaidia soka la Tanzania kusonga mbele.

Kayuni amewatahadharisha kuwa wanapochezesha vibaya wanajiharibia wao wenyewe, kwani mchezo wa soka una mashabiki wengine na unaonyeshwa karibu kila sehemu kutokana na teknolojia kukua.
Hawa ni baadhi ya waamuzi kuwa wakiwa wanapasha moto mwili

"Endapo mtarubuniwa na viongozi wa vyama vya soka FA wanapokwenda kuchezesha mtoe taarifa kwa maandishi katika  ofisi yangu itawashughulikie kulikoni waamuzi kuendelea kuumia au kuwa mbuzi wa kafara," alisema Kayuni.

Hata hivyo, alisema amekuwa akisikia malalamiko kwa pembeni, lakini hajafikishiwa kwake.
Alisema amepata taarifa kuwa wanapokwenda mikoani kuchezesha viongozi wa FA wanawashinikiza timu zao zishinde na mnapoacha kutekeleza matakwa yao wanawanyima posho zao.

Jumla ya waamuzi wapatao 190 kutoka mikoa yote wameudhuria semina na kufanya mtihani ya utimamu  wa mwili. Semina hii inaratajiwa kufungwa kesho jioni.
ROCKERSPORTS UNDERSTAND

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers