HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

20 October 2012

KUTOKA 2 BILA HADI TATU MBILI



YANGA SC leo imetoka nyuma kwa mabao 2-0 na kushinda 3-2 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga itemize pointi 14, baada ya kucheza mechi nane, hivyo kujiweka sawa katika nafasi ya tatu, ikizidwa pointi tatu na Azam inayoshika nafasi ya pili na pointi nne na Simba inayoongoza ligi hiyo.
Hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimekwishafungana mabao 2-2, Ruvu Shooting wakitangulia na baadaye Yanga kusawazisha.
Mabao ya Ruvu yalifungwa na mshambuliaji Seif Abdallah dakika ya tatu na lingine dakika ya 10, yote kutokana na mipira kutoka upande wa kulia mwa Uwanja, la kwanza mpira wa adhabu na la pili krosi.
Rashid Gumbo aliangushwa nje kidogo ya eneo la hatari na Mbuyu Twite akaenda kupiga mpira wa adhabu uliotinga moja kwa moja nyavuni dakika ya 20 na haraka haraka Jerry Tegete akauchukua mpira kwenye nyavu za Ruvu na kwenda kuuweka katikati.
Jeryson Tegete akishangilia bao alilofunga
pallanyor.blogpcha
Hilo lilikuwa bao la pili Twite anaifungia Yanga kwenye ligi, ndani ya mechi nane alizocheza.
Kipindi cha pili Yanga walirudi na kasi tena na kufanikiwa kupata bao la ushindi dakika ya 65, ambalo lilifungwa na Kavumbangu.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Coastal Union iliifunga Mtibwa Sugar mabao 3-1 mabao ya Juma Jabu, Daniel Lyanga na Lameck Dayton, la Mtibwa lilifungwa na Shaaban Nditi.

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers