HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

20 October 2012

Wanyama ALA NYAMA USKOCHI

Victor Wanyama 


Mkenya, Victor Wanyama amefunga mabao mawili kwa kuisadia klabu yake ya Celtic kuinyeshea klabu ya St. Mirren kwa mabao 5-0, na kuendeleza uongozi wao katika ligi kuu ya premier nchini Scotland.
Ushindi huo umeipa Celtic matumaini makubwa huku ikijiandaa kwa michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa barani ulaya dhidi ya Barcelona.
Hata hivyo, St Mirren ilipoteza nafasi nyingi za kufunga wakati wa mechi hiyo. Garry Hooper aliifungia celtic bao lake la kwanza kunako dakika ya kumi na tano kabla ya Efe Ambrose kufungwa bao la pili.
Wanyama naye akafunga bao la tatu kunako dakika ya 32 na dakika chache baadaye Wanyama aklafunga bao la pili.
Kocha wa St Mirren Danny Lennon amesema amehuzunishwa sana na matokeo ya mechi hiyo, kwani wachezaji wake hawakucheza kama kawaida yao.
Lakini kocha wa Celtic, Neil Lennon amesema mechi hiyo imekuwa fursa nzuri kwa wachezaji wake kujiandaa kwa mechi yao ya wiki ijayo dhidi ya Barcelona



No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers