HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

28 October 2012

PONGEZI KWA UONGOZI MPYA SIMIYU FA




Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Simiyu (SIFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Oktoba 27 mwaka huu).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa SIFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Simiyu.
TFF inaahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Kamati ya Utendaji ya SIFA ambayo ndiyo ya kwanza kuchaguliwa katika mkoa huo mpya chini ya uenyekiti wa Epafra Swai.
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu Simiyu kwa kuzingatia katiba ya SIFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya SIFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa ni Epafra Swai (Mwenyekiti), Kahema Manyili (Makamu Mwenyekiti), Sosie Chalamila (Katibu Msaidizi), Shabani Mwiko Aziz (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF) na Thomson Mtani (Mwakilishi wa Klabu TFF).

No comments:

Post a Comment

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers